Yeremia 3

Israeli Asiye Mwaminifu

1 “Kama mtu akimpa talaka mkewe,

naye akamwacha na akaolewa na mtu mwingine,

je, huyo mume aweza kumrudia tena?

Je, hiyo nchi haitanajisika kabisa?

Lakini umeishi kama kahaba na wapenzi wengi:

je, sasa utanirudia tena?”

asemaBwana.

2 “Inua macho utazame miinuko iliyo kame na uone.

Je, pana mahali ambapo hawajalala nawe?

Uliketi kando ya barabara ukiwasubiri wapenzi,

ukakaa kama yeye ahamahamaye jangwani.

Umeinajisi nchi

kwa ukahaba wako na uovu wako.

3 Kwa hiyo mvua imezuiliwa,

wala mvua za vuli hazikunyesha.

Hata hivyo, una uso wa shaba kama wa kahaba;

unakataa kutahayari kwa aibu.

4 Je, wewe hujaniita hivi punde tu:

‘Baba yangu, rafiki yangu tangu ujana wangu,

5 je, utakasirika siku zote?

Je, ghadhabu yako itaendelea milele?’

Hivi ndivyo unavyozungumza,

lakini unafanya maovu yote uwezayo.”

Wito Kwa Ajili Ya Toba

6 Wakati wa utawala wa Mfalme Yosia,Bwanaaliniambia, “Umeona kile ambacho Israeli asiyemwaminifu alichofanya? Amepanda juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila mti uliotanda na amefanya uzinzi huko.

7 Mimi nilifikiri kuwa baada ya kuyafanya yote haya angelinirudia lakini hakurudi, naye dada yake Yuda asiye mwaminifu aliona hili.

8 Nilimpa Israeli asiye mwaminifu hati yake ya talaka na kumfukuza kwa ajili ya uzinzi wake wote. Hata hivyo nikaona kuwa Yuda dada yake asiyemwaminifu hakuogopa, pia alitoka na kufanya uzinzi.

9 Kwa sababu uasherati wa Israeli haukuwa kitu kwake aliinajisi nchi kwa kuzini na jiwe na mti.

10 Pamoja na hayo yote, Yuda dada yake ambaye si mwaminifu hakunirudia kwa moyo wake wote, bali kwa kujifanya tu,” asemaBwana.

11 Bwanaakaniambia, “Israeli asiye mwaminifu ana haki kuliko Yuda aliye mdanganyifu.

12 Nenda, ukatangaze ujumbe huu kuelekea kaskazini:

“ ‘Rudi, Israeli usiye mwaminifu,’ asemaBwana,

‘sitakutazama tena kwa uso uliokunjamana,

kwa kuwa mimi ni mwenye huruma,’ asemaBwana,

‘Sitashika hasira yangu milele.

13 Ungama dhambi zako tu:

kwamba umemwasiBwanaMungu wako,

umetapanya wema wako kwa miungu ya kigeni

chini ya kila mti unaotanda,

nawe hukunitii mimi,’ ”

asemaBwana.

14 “Rudini, enyi watu msio waaminifu, kwa kuwa mimi ni mume wenu,” asemaBwana. “Nitawachagua ninyi, mmoja kutoka kwenye mji na wawili kutoka kwenye ukoo, nami nitawaleta Sayuni.

15 Kisha nitawapeni wachungaji wanipendezao moyo wangu ambao watawaongoza kwa maarifa na ufahamu.

16 Katika siku hizo, idadi yenu itakapokuwa imeongezeka sana katika nchi, watu hawatasema tena ‘Sanduku la Agano laBwana,’ ” asemaBwana. “Halitaingia tena kwenye mawazo yao wala kukumbukwa, hawatalihitaji wala halitatengenezwa jingine.

17 Wakati huo, watapaita Yerusalemu kiti cha enzi chaBwana, nayo mataifa yote watakusanyika Yerusalemu kuliheshimu jina laBwana. Hawatafuata tena ukaidi wa mioyo yao miovu.

18 Katika siku hizo, nyumba ya Yuda itaungana na nyumba ya Israeli, wao kwa pamoja watakuja kutoka nchi ya kaskazini kwenda kwenye nchi niliyowapa baba zenu kama urithi.

19 “Mimi mwenyewe nilisema,

“ ‘Tazama jinsi nitakavyowatunza kwa furaha kama wana

na kuwapa nchi nzuri,

urithi ulio mzuri kuliko wa taifa jingine lo lote.’

Nilidhani mngeniita ‘Baba’

na kwamba msingegeuka, mkaacha kunifuata.

20 Lakini kama mwanamke asiye mwaminifu kwa mumewe,

vivyo hivyo mmekosa uaminifu kwangu pia, Ee nyumba ya Israeli,”

asemaBwana.

21 Kilio kinasikika juu ya miinuko iliyo kame,

kulia na kuomboleza kwa watu wa Israeli,

kwa sababu wamepotoka katika njia zao

na wamemsahauBwanaMungu wao.

22 “Rudini, enyi watu msio waaminifu,

nami nitawaponya ukengeufu wenu.”

“Naam, tutakujia

kwa maana wewe niBwanaMungu wetu.

23 Hakika zile ghasia za kuabudu sanamu kwenye vilima

na milimani ni udanganyifu;

hakika katikaBwana, Mungu wetu,

uko wokovu wa Israeli.

24 Tangu ujana wetu miungu ya aibu imeyala

matunda ya kazi za baba zetu:

makundi yao ya kondoo na mbuzi, pamoja na ng’ombe,

wana wao na binti zao.

25 Sisi na tulale chini katika aibu yetu,

fedheha yetu na itufunike.

Tumetenda dhambi dhidi yaBwanaMungu wetu,

sisi na mababa zetu;

tangu ujana wetu hadi leo

hatukumtiiBwanaMungu wetu.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/3-917b6ea650bc5f87169f2d50b31289b1.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

1 × 1 =