Yeremia 24

Vikapu Viwili Vya Tini

1 Baada ya Yekoniamwana wa Yehoyakimumfalme wa Yuda pamoja na maafisa, mafundi stadi na wahunzi wa Yuda kuchukuliwa kutoka Yerusalemu kwenda Babeli na Nebukadneza mfalme wa Babeli kwenda uhamishoni huko Babeli,Bwanaakanionyesha vikapu viwili vya tini vilivyowekwa mbele ya Hekalu laBwana.

2 Kikapu kimoja kilikuwa na tini nzuri sana, kama zile za mavuno ya kwanza, kikapu cha pili kilikuwa na tini dhaifu sana, mbaya mno zisizofaa kuliwa.

3 KishaBwanaakaniuliza, “Je, Yeremia unaona nini?”

Nikamjibu, “Ninaona tini zile zilizo nzuri, ni nzuri sana, lakini zilizo dhaifu, ni mbaya mno zisizofaa kuliwa.”

4 Kisha neno laBwanalikanijia:

5 “Hili ndiloBwana, Mungu wa Israeli asemalo: ‘Kama zilivyo hizi tini nzuri, ndivyo ninavyowaona kuwa bora watu wa uhamisho kutoka Yuda, niliowaondoa kutoka mahali hapa kwenda katika nchi ya Wakaldayo.

6 Macho yangu yatakuwa juu yao kwa ajili ya kuwapatia mema, nami nitawarudisha tena katika nchi hii. Nitawajenga wala sitawabomoa, nitawapanda wala sitawang’oa,

7 nitawapa moyo wa kunifahamu mimi, kwamba mimi ndimiBwana. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao, kwa maana watanirudia kwa moyo wao wote.

8 “ ‘Lakini kama zilivyo zile tini dhaifu, ambazo ni mbaya mno zisizofaa kuliwa,’ asemaBwana, ‘ndivyo nitakavyomtendea Sedekia mfalme wa Yuda, maafisa wake na mabaki wengine kutoka Yerusalemu, kwamba wamebaki katika nchi hii au wanaishi Misri.

9 Nitawafanya kuwa chukizo kabisa na kitu cha kulaumiwa katika mataifa yote ya dunia, watakuwa aibu na kitu cha kudharauliwa, chombo cha dhihaka na kulaaniwa, po pote nitakakowafukuzia.

10 Nitautuma upanga, njaa na tauni dhidi yao mpaka wawe wameangamia kutoka nchi niliyowapa wao na baba zao.’ ”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/24-470e55bc0d3f7a0e53c096330bff09fb.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

eighteen − 7 =