Furaha Ya Kweli
1 Heri mtu yule ambaye
haendi katika shauri la watu waovu,
wala hakusimama katika njia ya wenye dhambi
au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 Bali huifurahia sheria yaBwana,
naye huitafakari hiyo sheria mchana na usiku.
3 Mtu huyo ni kama mti uliopandwa
kando ya vijito vya maji,
ambao huzaa matunda kwa majira yake
na majani yake hayanyauki.
Lo lote afanyalo hufanikiwa.
Huzuni Ya Waovu
4 Sivyo walivyo waovu!
Wao ni kama makapi
yapeperushwayo na upepo.
5 Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu,
wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 Kwa maanaBwanahuziangalia njia za mwenye haki,
bali njia ya waovu itaangamia.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/1-461588185b7df957126ca69dd341074d.mp3?version_id=1627—