Zaburi 2

Mfalme Aliyechaguliwa Na Mungu

1 Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya,

na mataifa kula njama bure?

2 Wafalme wa dunia wanajipanga

na watawala wanajikusanya pamoja

dhidi yaBwana

na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.

3 Wanasema, “Tuvunje minyororo yao

na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”

4 Yeye atawalaye mbinguni hucheka,

Bwana huwadharau.

5 Kisha huwakemea katika hasira yake

na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,

6 “Nimemtawaza mfalme wangu

juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”

Ushindi Wa Mfalme

7 Nitatangaza amri yaBwana:

Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu,

leo mimi nimekuzaa.

8 Niombe, nami nitayafanya mataifa

kuwa urithi wako,

miisho ya dunia kuwa milki yako.

9 Utawatawala kwa fimbo ya kifalme ya chuma

na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”

10 Kwa hiyo, ninyi wafalme, iweni na hekima;

mwonyeke, enyi watawala wa dunia.

11 MtumikieniBwanakwa hofu

na mshangilieni kwa kutetemeka.

12 Mbusu Mwana, asije akakasirika

nawe ukaangamizwa katika njia yako,

kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula.

Heri wote wanaomkimbilia.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/2-a11c6bc14963afae6c73d8884c7251e0.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

nine − one =