Kumtumaini Bwana
(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)
1 KwaBwananinakimbilia,
unawezaje basi kuniambia:
“Ruka kama ndege kwenye mlima wako.
2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao,
huweka mishale kwenye uzi wake,
wakiwa gizani ili kuwapiga
wanyofu wa moyo.
3 Wakati misingi imeharibiwa,
mwenye haki anaweza kufanya nini?”
4 Bwanayuko ndani ya Hekalu lake takatifu;
Bwanayuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni.
Huwaangalia wana wa watu,
macho yake yanawajaribu.
5 Bwanahuwajaribu wenye haki,
lakini waovu na wale wanaopenda jeuri
nafsi yake huwachukia.
6 Juu ya waovu atawanyeshea makaa ya moto mkali
na kiberiti kinachowaka,
upepo wenye joto kali ndio fungu lao.
7 Kwa kuwaBwanani mwenye haki,
hupenda haki;
watu wanyofu watauona uso wake.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/11-5c07d8f7f91202ea2f0e5f2cfada8510.mp3?version_id=1627—