Zaburi 11

Kumtumaini Bwana

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)

1 KwaBwananinakimbilia,

unawezaje basi kuniambia:

“Ruka kama ndege kwenye mlima wako.

2 Hebu tazama, waovu wanapinda pinde zao,

huweka mishale kwenye uzi wake,

wakiwa gizani ili kuwapiga

wanyofu wa moyo.

3 Wakati misingi imeharibiwa,

mwenye haki anaweza kufanya nini?”

4 Bwanayuko ndani ya Hekalu lake takatifu;

Bwanayuko kwenye kiti chake cha enzi mbinguni.

Huwaangalia wana wa watu,

macho yake yanawajaribu.

5 Bwanahuwajaribu wenye haki,

lakini waovu na wale wanaopenda jeuri

nafsi yake huwachukia.

6 Juu ya waovu atawanyeshea makaa ya moto mkali

na kiberiti kinachowaka,

upepo wenye joto kali ndio fungu lao.

7 Kwa kuwaBwanani mwenye haki,

hupenda haki;

watu wanyofu watauona uso wake.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/11-5c07d8f7f91202ea2f0e5f2cfada8510.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

twelve + nine =