Zaburi 12

Kuomba Msaada

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Sheminithi: Zaburi Ya Daudi)

1 Bwanatusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka;

waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.

2 Kila mmoja humwambia jirani yake uongo;

midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.

3 Bwanana akatilie mbali midomo yote ya hila

na kila ulimi uliojaa majivuno

4 ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda;

midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”

5 “Kwa sababu ya uonevu wa wanyonge

na kulia kwa uchungu kwa wahitaji,

nitainuka sasa,” asemaBwana.

“Nitawalinda kutokana na wale

wenye nia mbaya juu yao.”

6 Maneno yaBwanani safi,

kama fedha iliyosafishwa katika tanuru,

iliyosafishwa mara saba.

7 EeBwana, utatuweka salama

na kutulinda na kizazi hiki milele.

8 Watu waovu huenda wakiringa kila mahali

wakati ambapo yule aliye mbaya sana

ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/12-78f49a641ddd6c81699450d676c86446.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

two × four =