Kuomba Msaada
(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Sheminithi: Zaburi Ya Daudi)
1 Bwanatusaidie, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka;
waaminifu wametoweka miongoni mwa wanadamu.
2 Kila mmoja humwambia jirani yake uongo;
midomo yao ya hila huzungumza kwa udanganyifu.
3 Bwanana akatilie mbali midomo yote ya hila
na kila ulimi uliojaa majivuno
4 ule unaosema, “Kwa ndimi zetu tutashinda;
midomo ni mali yetu, bwana wetu ni nani?”
5 “Kwa sababu ya uonevu wa wanyonge
na kulia kwa uchungu kwa wahitaji,
nitainuka sasa,” asemaBwana.
“Nitawalinda kutokana na wale
wenye nia mbaya juu yao.”
6 Maneno yaBwanani safi,
kama fedha iliyosafishwa katika tanuru,
iliyosafishwa mara saba.
7 EeBwana, utatuweka salama
na kutulinda na kizazi hiki milele.
8 Watu waovu huenda wakiringa kila mahali
wakati ambapo yule aliye mbaya sana
ndiye anayeheshimiwa miongoni mwa watu.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/12-78f49a641ddd6c81699450d676c86446.mp3?version_id=1627—