Maombi Ya Kuhifadhiwa Dhidi Ya Uovu
(Zaburi Ya Daudi)
1 EeBwana, ninakuita wewe,
uje kwangu hima.
Sikia sauti yangu ninapokuita.
2 Maombi yangu na yafike mbele zako
kama uvumba;
kuinua mikono yangu juu
na kuwe kama dhabihu ya jioni.
3 EeBwana, weka mlinzi kinywani mwangu,
weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
4 Usiuache moyo wangu uvutwe katika lililo baya,
nisije nikashiriki katika matendo maovu
pamoja na watu watendao mabaya,
wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
5 Mtu mwenye haki na anipige:
ni jambo la huruma;
na anikemee,
ni mafuta kichwani mwangu.
Kichwa changu hakitalikataa.
Hata hivyo, maombi yangu daima
ni kinyume cha watenda mabaya,
6 watawala wao watatupwa chini
kutoka kwenye majabali,
waovu watajifunza kwamba maneno yangu
yalikuwa kweli.
7 Watasema, “Kama mtu anavyolima
na kuvunja ardhi,
ndivyo mifupa yetu imetawanywa
kwenye mlango wa kaburi.”
8 Lakini nimekaza macho yangu kwako,
EeBwanaMwenyezi,
ndani yako nimekimbilia,
usiniache nife.
9 Niepushe na mitego waliyonitegea,
kutokana na mitego
iliyotegwa na watenda mabaya.
10 Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe,
wakati mimi ninapita salama.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/141-2e78f72da3c85efe3c132cabfafda772.mp3?version_id=1627—