Zaburi 142

Maombi Ya Kuokolewa Dhidi Ya Watesi

(Utenzi Wa Daudi Alipokuwa Pangoni. Maombi)

1 NamliliaBwanakwa sauti kubwa,

nainua sauti yangu kwaBwanaanihurumie.

2 Namimina malalamiko yangu mbele zake,

mbele zake naeleza shida zangu.

3 Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu,

wewe ndiwe unajua njia zangu.

Katika njia ninayopita

watu wameweka mtego

kwa ajili yangu.

4 Tazama kuume kwangu na uone,

hakuna hata mmoja anayejihusisha nami.

Sina kimbilio,

hakuna anayejali maisha yangu.

5 EeBwana, nakulilia wewe,

nasema, “Wewe ni kimbilio langu,

fungu langu katika nchi ya walio hai.”

6 Sikiliza kilio changu,

kwa sababu mimi ni mhitaji sana;

niokoe na wale wanaonifuatilia,

kwa kuwa wamenizidi nguvu.

7 Nifungue kutoka katika kifungo changu,

ili niweze kulisifu jina lako.

Ndipo wenye haki watanizunguka,

kwa sababu ya wema wako kwangu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/142-016a7e0786320f3f02f0ea5ebd0aba8f.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

four × 2 =