Maombi Ya Kuokolewa Dhidi Ya Watesi
(Utenzi Wa Daudi Alipokuwa Pangoni. Maombi)
1 NamliliaBwanakwa sauti kubwa,
nainua sauti yangu kwaBwanaanihurumie.
2 Namimina malalamiko yangu mbele zake,
mbele zake naeleza shida zangu.
3 Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu,
wewe ndiwe unajua njia zangu.
Katika njia ninayopita
watu wameweka mtego
kwa ajili yangu.
4 Tazama kuume kwangu na uone,
hakuna hata mmoja anayejihusisha nami.
Sina kimbilio,
hakuna anayejali maisha yangu.
5 EeBwana, nakulilia wewe,
nasema, “Wewe ni kimbilio langu,
fungu langu katika nchi ya walio hai.”
6 Sikiliza kilio changu,
kwa sababu mimi ni mhitaji sana;
niokoe na wale wanaonifuatilia,
kwa kuwa wamenizidi nguvu.
7 Nifungue kutoka katika kifungo changu,
ili niweze kulisifu jina lako.
Ndipo wenye haki watanizunguka,
kwa sababu ya wema wako kwangu.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/142-016a7e0786320f3f02f0ea5ebd0aba8f.mp3?version_id=1627—