Zaburi 150

Msifuni Bwana Kwa Ukuu Wake

1 MsifuniBwana.

Msifuni Mungu katika patakatifu pake,

msifuni katika mbingu zake kuu.

2 Msifuni kwa matendo yake makuu,

msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

3 Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta,

msifuni kwa kinubi na zeze,

4 Msifuni kwa matari na kucheza,

msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,

5 Msifuni kwa matoazi yaliayo,

msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6 Kila chenye pumzi na kimsifuBwana.

MsifuniBwana. Haleluya!

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/150-cc95c5b1e920e3320c0de853056acb58.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

8 + 13 =