Zaburi 149

Wimbo Wa Kumsifu Mungu Kwa Wema Wake

1 MsifuniBwana.

MwimbieniBwanawimbo mpya,

sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.

2 Israeli na washangilie katika Muumba wao,

watu wa Sayuni na wafurahi katika mfalme wao.

3 Na walisifu jina lake kwa kucheza

na wampigie muziki kwa matari na kinubi.

4 Kwa maanaBwanaanapendezwa na watu wake,

anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.

5 Watakatifu na washangilie katika heshima hii

na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.

6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao

na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,

7 ili walipize mataifa kisasi

na adhabu juu ya mataifa,

8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo,

wakuu wao kwa pingu za chuma,

9 ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao.

Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote.

MsifuniBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/149-61e7d4fbad63268e796907d56d248b66.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

5 × 3 =