Wimbo Wa Kumsifu Mungu Kwa Wema Wake
1 MsifuniBwana.
MwimbieniBwanawimbo mpya,
sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
2 Israeli na washangilie katika Muumba wao,
watu wa Sayuni na wafurahi katika mfalme wao.
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza
na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
4 Kwa maanaBwanaanapendezwa na watu wake,
anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
5 Watakatifu na washangilie katika heshima hii
na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.
6 Sifa za Mungu na ziwe vinywani mwao
na upanga ukatao kuwili mikononi mwao,
7 ili walipize mataifa kisasi
na adhabu juu ya mataifa,
8 wawafunge wafalme wao kwa minyororo,
wakuu wao kwa pingu za chuma,
9 ili kuwafanyia hukumu iliyoandikwa dhidi yao.
Huu ndio utukufu wa watakatifu wake wote.
MsifuniBwana.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/149-61e7d4fbad63268e796907d56d248b66.mp3?version_id=1627—