Zaburi 16

Sala ya Matumaini

(Utenzi wa Daudi)

1 Ee Mungu, uniweke salama,

kwa maana kwako nimekimbilia.

2 NilimwambiaBwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu;

pasipo wewe sina jambo jema.”

3 Kwa habari ya watakatifu walioko duniani,

ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.

4 Huzuni itaongezeka kwa wale

wanaokimbilia miungu mingine.

Sitazimimina sadaka zao za damu

au kutaja majina yao midomoni mwangu.

5 Bwanaumeniwekea fungu langu na kikombe changu;

umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.

6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri,

hakika nimepata urithi mzuri.

7 NitamsifuBwanaambaye hunishauri,

hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.

8 NimemwekaBwanambele yangu daima.

Kwa kuwa yupo mkono wangu wa kuume,

sitatikiswa.

9 Kwa hiyo moyo wangu una furaha na ulimi wangu unashangilia;

pia mwili wangu utapumzika salama,

10 kwa sababu hutanitelekeza kuzimu,

wala hutaacha Mtakatifu Wako aone uharibifu.

11 Umenijulisha njia ya uzima;

utanijaza na shangwe katika uwepo wako,

pamoja na furaha za milele

katika mkono wako wa kuume.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/16-4ccaddf1574a9e1359b06bd28e2a0236.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

one × 3 =