Zaburi 15

Kitu Mungu Anachotaka

(Zaburi Ya Daudi)

1 Bwana, ni nani awezaye kukaa

katika Hekalu lako?

Nani awezaye kuishi

katika mlima wako mtakatifu?

2 Ni yule aendaye pasipo mawaa,

anayetenda yaliyo haki,

asemaye kweli toka moyoni mwake

3 na hana masingizio ulimini mwake,

asiyemtenda jirani yake vibaya

na asiyemsingizia mwenzake,

4 ambaye humdharau mtu mbaya sana,

lakini huwaheshimu wale

ambao humwogopaBwana,

yule atunzaye kiapo chake

hata kama anaumia.

5 Yeye akopeshaye fedha yake bila riba,

na hapokei rushwa

dhidi ya mtu asiye na hatia.

Mtu afanyaye haya

kamwe hatatikisika.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/15-12ac0bb687ff8678dd16cf5435ddfab1.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

20 − six =