Kuomba Msaada
(Zaburi Ya Daudi)
1 Ninakuita wewe, EeBwana, Mwamba wangu;
usiwe kwangu kama kiziwi.
Kwa sababu ukinyamaza
nitafanana na hao
waliokwisha shuka shimoni.
2 Sikia kilio changu unihurumie
ninapokuita kwa ajili ya msaada,
niinuapo mikono yangu kuelekea
Patakatifu pa Patakatifu pako.
3 Usiniburute pamoja na waovu,
pamoja na hao watendao mabaya,
ambao huzungumza na jirani zao
maneno mazuri,
lakini mioyoni mwao wameficha chuki.
4 Uwalipe sawasawa na matendo yao,
sawasawa na matendo yao maovu;
walipe sawasawa na kazi za mikono yao,
uwalipe wanavyostahili.
5 Kwa kuwa hawaheshimu kazi zaBwana,
na yale ambayo mikono yake imetenda,
atawabomoa na kamwe
hatawajenga tena.
6 Bwanaasifiwe,
kwa maana amesikia kilio changu
nikimwomba anihurumie.
7 Bwanani nguvu zangu na ngao yangu,
moyo wangu umemtumaini yeye,
nami nimesaidiwa.
Moyo wangu unarukaruka kwa furaha
nami nitamshukuru kwa wimbo.
8 Bwanani nguvu ya watu wake,
ngome ya wokovu kwa mpakwa mafuta wake.
9 Waokoe watu wako na uubariki urithi wako;
uwe mchungaji wao na uwabebe milele.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/28-ccdd4c1f15c10ab12f79c0f60d9b93a3.mp3?version_id=1627—