Sauti Ya Bwana Wakati Wa Dhoruba
(Zaburi Ya Daudi)
1 MpeniBwanaEnyi mashujaa,
mpeniBwanautukufu na nguvu.
2 MpeniBwanautukufu unaostahili jina lake;
mwabuduniBwanakatika uzuri
wa utakatifu wake.
3 Sauti yaBwanaiko juu ya maji;
Mungu wa utukufu hupiga radi,
Bwanahupiga radi juu ya maji makuu.
4 Sauti yaBwanaina nguvu;
sauti yaBwanani tukufu.
5 Sauti yaBwanahuvunja mierezi;
Bwanahuvunja vipande vipande
mierezi ya Lebanoni.
6 Hufanya Lebanoni irukaruke kama ndama,
# Sirioniurukaruke kama mwana nyati.
7 Sauti yaBwanahupiga kwa miali
ya umeme wa radi.
8 Sauti yaBwanahutikisa jangwa;
Bwanahutikisa Jangwa la Kadeshi.
9 Sauti yaBwanahuzalisha ayala,
na huuacha msitu wazi.
Hekaluni mwake wote wasema,
“Utukufu!”
10 Bwanahuketi akiwa ametawazwa juu ya gharika;
Bwanaametawazwa
kuwa Mfalme milele.
11 Bwanahuwapa watu wake nguvu;
Bwanahuwabariki watu wake
kwa kuwapa amani.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/29-a77bafb769001fb1643ac0ddcb064950.mp3?version_id=1627—