Zaburi 4

Sala Ya Jioni Ya Kuomba Msaada

(Kwa Mwimbishaji: Kwa Ala Za Nyuzi Za Muziki. Zaburi Ya Daudi)

1 Unijibu nikuitapo,

Ee Mungu wangu mwenye haki!

Unipumzishe katika shida zangu,

nirehemu, usikie ombi langu.

2 Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu

kuwa aibu mpaka lini?

Mtapenda udanganyifu

na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?

3 Fahamuni hakika kwambaBwanaamewatenga

wale wamchao kwa ajili yake;

Bwanaatanisikia nimwitapo.

4 Katika hasira yako usitende dhambi,

mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya

mkiichunguza mioyo yenu.

5 Toeni dhabihu iliyo sahihi

na mumtegemeeBwana.

6 Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye

kutuonyesha jema lo lote?”

EeBwana, utuangazie nuru ya uso wako.

7 Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa

kuliko watu waliopata ngano na divai kwa wingi.

8 Nitajilaza chini na kulala kwa amani,

kwa kuwa wewe peke yako, EeBwana,

waniwezesha kukaa kwa salama.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/4-d29771b2637e4953932c84584e8c7c0e.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

14 + nine =