Sala Ya Jioni Ya Kuomba Msaada
(Kwa Mwimbishaji: Kwa Ala Za Nyuzi Za Muziki. Zaburi Ya Daudi)
1 Unijibu nikuitapo,
Ee Mungu wangu mwenye haki!
Unipumzishe katika shida zangu,
nirehemu, usikie ombi langu.
2 Enyi watu, mtabadilisha utukufu wangu
kuwa aibu mpaka lini?
Mtapenda udanganyifu
na kufuata miungu ya uongo mpaka lini?
3 Fahamuni hakika kwambaBwanaamewatenga
wale wamchao kwa ajili yake;
Bwanaatanisikia nimwitapo.
4 Katika hasira yako usitende dhambi,
mkiwa vitandani mwenu, mtulie kimya
mkiichunguza mioyo yenu.
5 Toeni dhabihu iliyo sahihi
na mumtegemeeBwana.
6 Wengi wanauliza, “Ni nani awezaye
kutuonyesha jema lo lote?”
EeBwana, utuangazie nuru ya uso wako.
7 Wewe umejaza moyo wangu kwa furaha kubwa
kuliko watu waliopata ngano na divai kwa wingi.
8 Nitajilaza chini na kulala kwa amani,
kwa kuwa wewe peke yako, EeBwana,
waniwezesha kukaa kwa salama.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/4-d29771b2637e4953932c84584e8c7c0e.mp3?version_id=1627—