Sala Ya Asubuhi Ya Kuomba Msaada
(Zaburi Ya Daudi Alipomkimbia Absalomu)
1 EeBwana, tazama adui zangu walivyo wengi!
Ni wengi kiasi gani wanaoinuka dhidi yangu!
2 Wengi wanasema juu yangu,
“Mungu hatamwokoa.”
3 Lakini wewe, EeBwana, ni ngao pande zote;
umeniwekea utukufu na kuinua kichwa changu.
4 NinamliliaBwanakwa sauti kuu,
naye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
5 Ninajilaza na kupata usingizi;
naamka tena, kwa maanaBwanahunitegemeza.
6 Sitaogopa makumi elfu ya adui,
wanaojipanga dhidi yangu kila upande.
7 EeBwana, amka!
Uniokoe, Ee Mungu wangu!
Wapige adui zangu wote kwenye taya,
vunja meno ya waovu.
8 Kwa maana wokovu watoka kwaBwana.
Baraka yako na iwe juu ya watu wako.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/3-02ebf1108eb4cf43d48b6134dc9a3fcb.mp3?version_id=1627—