2 Wafalme 11

Athalia Na Yoashi

1 Wakati Athalia mamaye Ahazia alipoona kwamba mwanawe amekufa, akainuka na kuiangamiza jamaa yote ya kifalme.

2 Lakini Yehosheba, binti wa Mfalme Yehoramu ambaye ni dada yake Ahazia, akamtwaa Yoashi mwana wa Ahazia kwa siri kutoka miongoni mwa wana wa kifalme, ambao walikuwa karibu kuuawa. Akamweka Yoashi pamoja na yaya wake ndani ya chumba cha kulala na kumficha humo ili Athalia asimwone; kwa hiyo hakuuawa.

3 Alibaki amefichwa pamoja na yaya wake kwenye Hekalu laBwanakwa miaka sita wakati Athalia alipokuwa akitawala nchi.

4 Katika mwaka wa saba Yehoyada kuhani akaamuru waletwe wakuu wa vikundi vya mamia wa Wakarina walinzi, nao wakaletwa kwake kwenye Hekalu laBwana. Akafanya agano nao na kuwaapisha katika Hekalu laBwana. Ndipo akawaonyesha mwana wa mfalme.

5 Akawaamuru akisema, “Hivi ndivyo iwapasavyo kufanya: Ninyi ambao mko makundi matatu mnaokwenda zamu siku ya Sabato, theluthi yenu itakuwa ikilinda jumba la kifalme,

6 theluthi nyingine italinda Lango la Suri, na theluthi nyingine italinda lango lililo nyuma ya walinzi, ambao hupeana zamu kulinda Hekalu;

7 nanyi ambao mko katika makundi mengine mawili ambao kwa kawaida hupumzika Sabato, wote mtalinda Hekalu kwa ajili ya mfalme.

8 Jipangeni kumzunguka mfalme, kila mtu akiwa na silaha yake mkononi mwake. Ye yote anayesogelea safu yenu ya askari ni lazima auawe. Kaeni karibu na mfalme po pote aendako.”

9 Majemadari wa vikosi vya mamia wakafanya sawasawa kama alivyoagiza kuhani Yehoyada. Kila mmoja akawachukua watu wake, wale waliokuwa wakienda zamu siku ya Sabato na wale waliokuwa katika mapumziko, nao wakaja kwa kuhani Yehoyada.

10 Ndipo akawapa wale majemadari mikuki na ngao zilizokuwa mali ya Mfalme Daudi na zile zilizokuwa ndani ya Hekalu laBwana.

11 Wale walinzi, kila mmoja akiwa na silaha yake mkononi mwake, wakajipanga kumzunguka mfalme, karibu na madhabahu na Hekalu, kuanzia upande wa kusini hadi upande wa kaskazini mwa Hekalu.

12 Yehoyada akamtoa mwana wa mfalme na kumvika taji, akampa nakala ya agano na kumtangaza kuwa mfalme. Wakamtia mafuta, nao watu wakapiga makofi na kupaza sauti wakisema, “Mfalme aishi maisha marefu!”

13 Athalia aliposikia kelele iliyofanywa na walinzi pamoja na watu, akawaendea watu pale penye Hekalu laBwana.

14 Akaangalia na tazama alikuwako mfalme, akiwa amesimama karibu na nguzo, kama ilivyokuwa desturi. Maafisa na wapiga tarumbeta walikuwa pembeni mwa mfalme, nao watu wote wa nchi walikuwa wakifurahi na kupiga tarumbeta. Kisha Athalia akararua majoho yake na kupiga kelele, “Uhaini! Uhaini!”

15 Kuhani Yehoyada akawaagiza majemadari wa vikosi vya mamia, waliokuwa wasimamizi wa jeshi, “Mleteni huyo Athalia nje katikati ya safu, na mtieni upanga mtu ye yote atakayemfuata.” Kwa kuwa kuhani alikuwa amesema, “Hatauawa ndani ya Hekalu laBwana.”

16 Basi wakamkamata Athalia na alipofika mahali ambapo farasi huingilia katika viwanja vya jumba la mfalme, wakamwulia hapo.

17 Ndipo Yehoyada akafanya Agano kati yaBwanana mfalme na watu kwamba watakuwa watu waBwana. Akafanya pia agano kati ya mfalme na watu.

18 Watu wote wa nchi wakaenda kwenye hekalu la Baali na kulibomoa. Wakavunja madhabahu zote na sanamu vipande vipande na kumwua Matani kuhani wa Baali mbele ya hiyo madhabahu.

Kisha Yehoyada kuhani akawaweka walinzi kwenye Hekalu laBwana.

19 Pamoja naye akawachukua majemadari wa mamia, Wakari, walinzi na watu wote wa nchi, nao kwa pamoja wakamshusha mfalme kutoka katika Hekalu laBwanana kwenda kwenye jumba la kifalme, wakiingilia njia ya lango la walinzi. Ndipo mfalme akachukua nafasi yake kwenye kiti cha enzi,

20 nao watu wote wa nchi wakafurahi. Mji ukatulia, kwa sababu Athalia alikuwa ameuawa kwa upanga huko kwenye jumba la kifalme.

21 Yoashi alikuwa na umri wa miaka saba wakati alipoanza kutawala.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/2KI/11-529a000ba40df9fc04897c306afddbef.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

1 × 5 =