Amosi 2

1 Hili ndilo asemaloBwana:

“Kwa dhambi tatu za Moabu,

hata kwa dhambi nne,

sitazuia ghadhabu yangu.

Kwa sababu alichoma mifupa ya mfalme wa Edomu,

ikawa kama chokaa.

2 Nitatuma moto juu ya Moabu

ambao utateketeza ngome ya Keriothi.

Moabu ataanguka kwa ghasia kubwa

katikati ya vilio vya vita na mlio wa tarumbeta.

3 Nitamwangamiza mtawala wake

na kuwaua maafisa wake wote pamoja naye,”

asemaBwana.

4 Hili ndilo asemaloBwana:

“Kwa dhambi tatu za Yuda,

hata kwa dhambi nne,

sitaizuia ghadhabu yangu.

Kwa sababu wameikataa sheria yaBwana

na hawakuzishika amri zake,

kwa sababu wamepotoshwa na miungu ya uongo,

miungu ambayo babu zao waliifuata.

5 Nitatuma moto juu ya Yuda

ambao utateketeza ngome za Yerusalemu.”

Hukumu Juu Ya Israeli

6 Hili ndilo asemaloBwana:

“Kwa dhambi tatu za Israeli,

hata kwa dhambi nne,

sitaizuia ghadhabu yangu.

Wanawauza wenye haki kwa fedha,

na maskini kwa jozi ya viatu.

7 Wanakanyaga juu ya vichwa vya maskini

kama vile juu ya mavumbi ya nchi

na kukataa haki kwa walioonewa.

Baba na mwanawe hushiriki msichana mmoja,

kwa hivyo hulinajisi Jina langu takatifu.

8 Watu hulala kando ya kila madhabahu

juu ya nguo zilizowekwa rehani.

Katika nyumba ya mungu wao hunywa mvinyo

ulionunuliwa kwa fedha walizotozwa watu.

9 “Nilimwangamiza Mwamori mbele yao,

ingawa alikuwa mrefu kama mierezi

na mwenye nguvu kama mialoni.

Niliyaangamiza matunda yake juu

na mizizi yake chini.

10 “Nilikupandisha toka Misri,

na nikawaongoza miaka arobaini jangwani

niwape nchi ya Waamori.

11 Pia niliinua manabii kutoka miongoni mwa wana wenu

na Wanadhiri kutoka miongoni

mwa vijana wenu wa kiume.

Je, hii si kweli, Enyi watu wa Israeli?”

asemaBwana.

12 “Lakini mliwafanya Wanadhiri kunywa mvinyo

na kuwaamuru manabii wasitoe unabii.

13 “Sasa basi, nitawaponda

kama gari lipondavyo

wakati limejazwa nafaka.

14 Mkimbiaji hodari hatanusurika,

wenye nguvu wataishiwa nguvu zao

na shujaa hataweza kuokoa maisha yake.

15 Mpiga upinde atakimbia,

askari wapiga mbio hawataweza kutoroka,

na mpanda farasi hataokoa maisha yake.

16 Hata askari walio mashujaa sana

siku hiyo watakimbia uchi,”

asemaBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/AMO/2-6a9e6bcc6ff37c87f934430ef4f642f7.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

seventeen + fourteen =