Maombolezo Na Wito Wa Toba
1 Sikia neno hili, Ee nyumba ya Israeli, ombolezo hili ninalifanya kuwahusu ninyi:
2 “Bikira Israeli ameanguka,
kamwe hatainuka tena,
ameachwa pweke katika nchi yake,
hakuna ye yote wa kumwinua.”
3 Hili ndiloBwanaMwenyezi asemalo:
“Wakati mmoja wa miji yako utakapopeleka watu elfu moja vitani,
mia moja tu watarudi;
wakati mji utakapopeleka mia moja,
kumi tu ndio watarudi hai.”
4 Hili ndiloBwanaasemalo kwa nyumba ya Israeli:
“Nitafuteni mpate kuishi,
5 Msitafute Betheli,
msiende Gilgali,
msisafiri kwenda Beer-Sheba.
Kwa maana kwa hakika Gilgali itakwenda uhamishoni,
# na Betheli itakuwa si kitu.”
6 MtafuteniBwanampate kuishi,
au atafagia nyumba ya Yosefu kama moto;
utawateketeza,
nayo Betheli haitakuwa
na ye yote wa kuuzima.
7 Ninyi ambao mnageuza haki kuwa uchungu
na kuiangusha haki chini
8 (yeye ambaye alifanya Kilimia na Orioni,
ambaye hugeuza giza kuwa mapambazuko
na mchana kuwa usiku,
ambaye huyaita maji ya bahari
na kuyamwaga juu ya uso wa nchi:
Bwanandilo jina lake;
9 yeye hufanya maangamizo kwenye ngome
na kufanya mji uliozungushiwa ngome kuwa ukiwa),
10 mnamchukia yule akemeaye mahakamani,
na kumdharau yule ambaye husema kweli.
11 Mnamgandamiza maskini
na kumlazimisha awape nafaka.
Kwa hiyo, ingawa mmejenga majumba ya mawe ya fahari,
hamtaishi ndani yake;
ingawa mmepanda mashamba mazuri ya mizabibu,
hamtakunywa divai yake.
12 Kwa kuwa ninajua hesabu ya makosa yenu
na ukubwa wa dhambi zenu.
Mmewaonea wenye haki na kupokea rushwa
na kuzuia haki ya maskini mahakamani.
13 Kwa hiyo mtu mwenye busara hunyamaza kimya
nyakati kama hizo,
kwa kuwa nyakati ni mbaya.
14 Tafuteni mema, wala si mabaya,
ili mpate kuishi.
NdipoBwanaMungu Mwenye Nguvu Zote
atakuwa pamoja nanyi,
kama msemavyo yupo nanyi.
15 Yachukieni maovu, yapendeni mema;
dumisheni haki mahakamani.
YamkiniBwanaMungu Mwenye Nguvu Zote
atawahurumia mabaki ya Yosefu.
16 Kwa hiyo hili ndilo Bwana,BwanaMungu Mwenye Nguvu Zote, asemalo:
“Kutakuwepo maombolezo katika barabara zote
na vilio vya uchungu
mahali pa njia kuu.
Wakulima wataitwa kuja kulia
na waombolezaji waje kuomboleza.
17 Kutakuwepo kuomboleza katika mashamba yote ya mizabibu,
kwa kuwa nitapita katikati yenu,”
asemaBwana.
Siku Ya Bwana
18 Ole wenu ninyi mnaoitamani
siku yaBwana!
Kwa nini mnaitamani siku yaBwana?
Siku hiyo itakuwa giza, si nuru.
19 Itakuwa kama vile mtu aliyemkimbia simba
kumbe akakutana na dubu,
kama vile mtu aliyeingia nyumbani mwake
na kuupumzisha mkono wake kwenye ukuta
kumbe akaumwa na nyoka.
20 Je, siku yaBwanahaitakuwa giza, na si nuru:
giza nene, bila mwonzi wa mwanga?
21 “Ninachukia, ninazidharau sikukuu zenu za dini;
siwezi kuvumilia makusanyiko yenu.
22 Hata ingawa mnaniletea sadaka zenu za kuteketezwa
na sadaka za nafaka,
sitazikubali.
Ingawa mnaniletea sadaka nzuri za amani,
sitazitambua.
23 Niondoleeni kelele za nyimbo zenu!
Sitasikiliza sauti za vinubi vyenu.
24 Lakini acheni haki itiririke kama mto,
na uadilifu uwe kama kijito kisichokauka!
25 “Je, mliniletea dhabihu na sadaka
mlipokuwa jangwani miaka arobaini,
Ee nyumba ya Israeli?
26 Mmeyainua madhabahu ya mfalme wenu:
Sikuthi mungu wenu mtawala,
Kiuni mungu wenu wa nyota;
ambao mliwatengeneza wenyewe.
27 Kwa sababu hiyo nitawapelekeni
uhamishoni mbali kupita Dameski,”
asemaBwana, ambaye jina lake
ni Mungu Mwenye Nguvu Zote.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/AMO/5-ee752d29b5071367ece5f6ff3b14473b.mp3?version_id=1627—