Isaya 12

Kushukuru Na Kusifu

1 Katika siku ile utasema:

“Nitakusifu wewe, EeBwana.

Ingawa ulinikasirikia,

hasira yako imegeukia mbali

nawe umenifariji.

2 Hakika Mungu ni wokovu wangu;

nitamtumaini wala sitaogopa.

Bwana,Bwana, ni nguvu zangu

na wimbo wangu;

amekuwa wokovu wangu.”

3 Kwa furaha mtachota maji

kutoka katika visima vya wokovu.

4 Katika siku hiyo mtasema:

“MshukuruniBwana, mliitie jina lake;

julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya,

tangazeni kuwa jina lake limetukuka.

5 MwimbieniBwana, kwa kuwa ametenda mambo makuu,

hili na lijulikane duniani kote.

6 Paza sauti uimbe kwa furaha, watu wa Sayuni,

kwa maana mkuu ni yeye

Aliye Mtakatifu wa Israeli miongoni mwenu.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/12-3cb1715dd81e8f1610a2b4da0e31be68.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

14 − nine =