Kushukuru Na Kusifu
1 Katika siku ile utasema:
“Nitakusifu wewe, EeBwana.
Ingawa ulinikasirikia,
hasira yako imegeukia mbali
nawe umenifariji.
2 Hakika Mungu ni wokovu wangu;
nitamtumaini wala sitaogopa.
Bwana,Bwana, ni nguvu zangu
na wimbo wangu;
amekuwa wokovu wangu.”
3 Kwa furaha mtachota maji
kutoka katika visima vya wokovu.
4 Katika siku hiyo mtasema:
“MshukuruniBwana, mliitie jina lake;
julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya,
tangazeni kuwa jina lake limetukuka.
5 MwimbieniBwana, kwa kuwa ametenda mambo makuu,
hili na lijulikane duniani kote.
6 Paza sauti uimbe kwa furaha, watu wa Sayuni,
kwa maana mkuu ni yeye
Aliye Mtakatifu wa Israeli miongoni mwenu.”
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/12-3cb1715dd81e8f1610a2b4da0e31be68.mp3?version_id=1627—