Isaya 25

Msifuni Bwana

1 EeBwana, wewe ni Mungu wangu,

nitakutukuza na kulisifu jina lako,

kwa maana katika ukamilifu wa uaminifu

umetenda mambo ya ajabu,

mambo yaliyokusudiwa tangu zamani.

2 Umeufanya mji kuwa lundo la kifusi,

mji wenye ngome kuwa magofu,

ngome imara ya wageni kuwa si mji tena,

wala hautajengwa tena kamwe.

3 Kwa hiyo mataifa yenye nguvu yatakuheshimu,

miji ya mataifa katili itakuheshimu wewe.

4 Umekuwa kimbilio la watu maskini,

kimbilio la mhitaji katika taabu yake,

hifadhi wakati wa dhoruba

na kivuli wakati wa hari.

Kwa maana pumzi ya wakatili

ni kama dhoruba ipigayo ukuta

5 na kama joto la jangwani.

Wewe wanyamazisha makelele ya wageni,

kama vile hari ipunguzwavyo na kivuli cha wingu,

ndivyo wimbo wa wakatili unyamazishwavyo.

6 Juu ya mlima huuBwanaMwenye Nguvu Zote ataandaa

karamu ya vinono kwa mataifa yote,

karamu ya mvinyo wa zamani,

nyama nzuri sana na divai zilizo bora sana.

7 Juu ya mlima huu ataharibu sitara ile ihifadhiyo mataifa yote,

kile kifuniko kifunikacho mataifa yote,

8 yeye atameza mauti milele katika ushindi.

BwanaMwenyezi atafuta machozi katika nyuso zote,

ataondoa aibu ya watu wake duniani kote.

Bwanaamesema hili.

9 Katika siku ile watasema,

“Hakika huyu ndiye Mungu wetu,

tuliyemtumaini naye akatuokoa.

Huyu ndiyeBwana, tuliyemtumaini;

sisi na tushangilie

na kufurahia katika wokovu wake.”

10 Mkono waBwanautatulia juu ya mlima huu,

bali Moabu atakanyagwa chini

kama majani makavu yakanyagwavyo kwenye shimo la mbolea.

11 Ingawa watakunjua mikono yao katikati yake,

kama vile mwogeleaji akunjuavyo mikono yake ili aogelee.

Mungu atashusha kiburi chao

licha ya ujanja wa mikono yao.

12 Atabomoa kuta ndefu za maboma yako

na kuziangusha chini,

atazishusha chini ardhini,

mpaka mavumbini kabisa.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/25-cd29ea3c711afef4cf9519ee40cb09d5.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

9 + six =