Isaya 26

Wimbo Wa Ushindi

1 Katika siku ile wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda:

Tuna mji ulio na nguvu,

Mungu huufanya wokovu kuwa kuta zake na maboma yake.

2 Fungua malango ili taifa lenye haki lipate kuingia,

taifa lile lishikalo imani.

3 Utamlinda katika amani kamilifu yeye ambaye

moyo wake ni thabiti

kwa sababu anakutumaini wewe.

4 MtumainiBwanamilele,

kwa kuwaBwana,Bwana,

ni Mwamba wa milele.

5 Huwashusha wale wajikwezao,

huushusha chini mji wenye kiburi,

huushusha hadi ardhini na kuutupa chini mavumbini.

6 Miguu hukanyaga chini,

miguu ya hao walioonewa,

hatua za hao maskini.

7 Mapito ya wenye haki yamenyooka,

Ewe uliye mwenye haki,

waisawazisha njia ya mtu mnyofu.

8 Naam,Bwanatukienenda katika sheria zako,

twakungojea wewe,

kulikumbuka jina lako

na sifa zako ndiyo shauku ya mioyo yetu.

9 Nafsi yangu yakutamani wakati wa usiku,

wakati wa asubuhi roho yangu yakuonea shauku.

Wakati hukumu zako zinapokuja juu ya dunia,

watu wa ulimwengu hujifunza haki.

10 Ingawa neema yaonyeshwa kwa waovu,

hawajifunzi haki,

hata katika nchi ya unyofu huendelea kutenda mabaya

wala hawaoni utukufu waBwana.

11 EeBwana, mkono wako umeinuliwa juu,

lakini hawauoni.

Wao na waone wivu wako kwa ajili ya watu wako tena waaibishwe,

moto uliowekwa akiba kwa ajili ya adui zako na uwateketeze.

12 Bwana, unaamuru amani kwa ajili yetu,

yale yote tuliyoweza kuyakamilisha

ni wewe uliyetenda kwa ajili yetu.

13 EeBwana, Mungu wetu, mabwana wengine zaidi ya wewe wametutawala,

lakini jina lako peke yako ndilo tunaloliheshimu.

14 Wao sasa wamekufa, wala hawako tena hai,

roho za waliokufa hazitarudi tena.

Uliwaadhibu na kuwaangamiza,

umefuta kumbukumbu lao lote.

15 Umeliongeza hilo taifa, EeBwana,

umeliongeza hilo taifa.

Umejipatia utukufu kwa ajili yako mwenyewe,

umepanua mipaka yote ya nchi.

16 Bwana, walikujia katika taabu yao,

wewe ulipowarudi,

waliweza kuomba kwa kunong’ona kwa shida sana.

17 Kama mwanamke mwenye mimba aliyekaribia kuzaa

anavyogaagaa na kulia kwa ajili ya maumivu yake,

ndivyo tulivyokuwa mbele zako, EeBwana.

18 Tulikuwa na mimba, tuligaagaa kwa maumivu,

lakini tulizaa upepo.

Hatukuleta wokovu duniani,

hatujazaa watu katika ulimwengu huu.

19 Lakini wafu wenu wataishi,

miili yao itafufuka.

Ninyi mnaokaa katika mavumbi,

amkeni mkapige kelele kwa furaha.

Umande wenu ni kama umande wa asubuhi,

dunia itawazaa wafu wake.

20 Nendeni, watu wangu, ingieni vyumbani mwenu

na mfunge milango nyuma yenu,

jificheni kwa kitambo kidogo

mpaka ghadhabu yake ipite.

21 Tazama,Bwanaanakuja kutoka katika makao yake

ili kuwaadhibu watu wa dunia kwa ajili ya dhambi zao.

Dunia itadhihirisha umwagaji damu juu yake,

wala haitaendelea kuwaficha watu wake waliouawa.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ISA/26-5e3fa261bb59ab57eddae9a43d7103c3.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

eighteen − 6 =