Kumbukumbu La Torati 8

Usimsahau Bwana

1 Uwe mwangalifu kufuata kila agizo ninalokupa wewe leo, ili mweze kuishi, kuongezeka na mweze kuingia mkamiliki nchi ambayoBwanaaliahidi kwa kiapo kwa baba zenu.

2 Kumbuka jinsiBwanaMungu wenu alivyowaongoza katika njia yote katika jangwa kwa miaka hii arobaini, kukunyenyekeza na kukujaribu ili ajue lililoko moyoni mwako, kwamba utayashika maagizo yake au la.

3 Alikudhili na kukufanya uone njaa kisha akulishe kwa mana, ambayo wewe wala baba zako hamkuijua, awafundishe kuwa mwanadamu hataishi kwa mkate tu bali kwa kila neno litokalo katika kinywa chaBwana.

4 Nguo zenu hazikuchakaa wala miguu yenu haikuvimba kwa miaka hii arobaini.

5 Mjue basi ndani ya mioyo yenu kama mtu anavyomwadibisha mwanawe, ndivyoBwanaMungu wako atawaadibisha ninyi.

6 Shikeni maagizo yaBwanaMungu wenu mtembee katika njia zake na kumheshimu.

7 Kwa kuwaBwanaMungu wenu anawaleta katika nchi nzuri, nchi yenye vijito na mabwawa ya maji, yenye chemchemi zinazotiririka mabondeni na katika vilima;

8 nchi yenye ngano na shayiri, mizabibu na mitini, mikomamanga, mafuta ya zeituni na asali;

9 nchi ambayo chakula hakitapungua na hamtakosa cho chote; nchi ambayo miamba yake ni chuma na mnaweza kuchimba shaba kutoka kwenye vilima.

10 Wakati mtakapokwisha kula na kushiba, msifuniBwanaMungu wenu kwa ajili ya nchi nzuri aliyowapa.

11 Jihadharini msimsahauBwanaMungu wenu, mkashindwa kushika maagizo yake, sheria na amri zake ambazo ninawapa leo.

12 Angalia wakati mtakapokuwa mmekula na kushiba, mkajenga nyumba nzuri na kukaa humo,

13 na wakati makundi yenu ya ng’ombe na mbuzi na kondoo yatakapoongezeka na fedha na dhahabu yenu itakapoongezeka na vyote mlivyo navyo vitakapozidishwa,

14 basi mioyo yenu isiwe na kiburi mkamsahauBwanaMungu wenu aliyewatoa katika nchi ya Misri, kutoka nchi ya utumwa.

15 Aliwaongoza kupitia jangwa lile kubwa na la kutisha, nchi ile ya kiu isiyo na maji, yenye nyoka wa sumu na nge. Aliwatolea maji kutoka kwenye mwamba mgumu.

16 Aliwapa mana ya kula jangwani, kitu ambacho baba zenu hawakukijua, ili kuwanyenyekesha na kuwajaribu ninyi ili mwishoni apate kuwatendea mema.

17 Mnaweza kusema, “Uwezo wangu na nguvu za mikono yangu ndizo zilizonipatia utajiri huu.”

18 Lakini kumbukeniBwanaMungu wenu, ndiye ambaye huwapa uwezo wa kupata utajiri, na hivyo kulithibitisha Agano lake, ambalo aliwaapia baba zenu, kama ilivyo leo.

19 Ikiwa mtamsahauBwanaMungu wenu, mkaifuata miungu mingine, mkaiabudu na kuisujudia, ninashuhudia dhidi yenu leo kwamba hakika mtaangamizwa.

20 Kama mataifaBwanaaliyoyaangamiza mbele yenu, ndivyo ninyi mtakavyoangamizwa kwa kutokumtiiBwanaMungu wenu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/DEU/8-8aca7ac071be4b88ae744c88841996b7.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

twelve − 4 =