Nahumu 1

1 Neno alilosema Mungu kuhusu Ninawi. Kitabu cha maono cha Nahumu, Mwelkoshi.

Hasira Ya Mungu Dhidi Ya Ninawi

2 Bwanani mwenye wivu na Mungu mlipiza kisasi;

Bwanahulipiza kisasi na amejaa ghadhabu.

Bwanahulipiza kisasi juu ya watesi wake,

naye anadumisha ghadhabu yake dhidi ya adui zake.

3 Bwanasi mwepesi wa hasira naye ni mwenye nguvu,

Bwanahataacha kuadhibu wenye hatia.

Njia yake ipo katika kisulisuli na tufani,

na mawingu ni vumbi la miguu yake.

4 Anakemea bahari na kuikausha,

anafanya mito yote kukauka.

Bashani na Karmeli zinanyauka

na maua ya Lebanoni hukauka.

5 Milima hutikisika mbele yake

na vilima huyeyuka.

Nchi hutetemeka mbele yake,

dunia na wote waishio ndani yake.

6 Ni nani awezaye kuzuia hasira yake yenye uchungu?

Nani awezaye kuvumilia hasira yake kali?

Ghadhabu yake imemiminwa kama moto,

na miamba inapasuka mbele zake.

7 Bwanani Mwema,

kimbilio wakati wa taabu.

Huwatunza wale wanaomtegemea,

8 lakini kwa mafuriko makubwa,

ataangamiza Ninawi;

atafuatilia adui zake hadi gizani.

9 Shauri baya lo lote wapangalo dhidi yaBwana

yeye atalikomesha;

taabu haitatokea mara ya pili.

10 Watasongwa katikati ya miiba

na kulewa kwa mvinyo wao.

Watateketezwa kama mabua makavu.

11 Ee Ninawi, kutoka kwako amejitokeza mmoja,

ambaye anapanga shauri baya

dhidi yaBwana

na kushauri uovu.

12 Hili ndilo asemaloBwana:

“Ingawa wana muungano nao ni wengi sana,

watakatiliwa mbali na kuangamia.

Ingawa nimekutesa wewe, Ee Yuda,

sitakutesa tena.

13 Sasa nitavunja nira zao kutoka katika shingo yako,

nami nitazivunjilia mbali pingu zako.”

14 Hii ndiyo amriBwanaaliyoitoa kukuhusu wewe, Ninawi:

“Hutakuwa na wazao

watakaoendeleza jina lako.

Nitaharibu sanamu za kuchonga na sanamu za kuyeyusha

ambazo zipo katika hekalu la miungu yenu.

Nitaandaa kaburi lako,

kwa maana wewe ni mwovu kabisa.”

15 Tazama, huko juu milimani,

miguu ya huyo mmoja aletaye habari njema,

ambaye anatangaza amani!

Ee Yuda, sheherekea sikukuu zako,

nawe utimize nadhiri zako.

Waovu hawatakuvamia tena;

wataangamizwa kabisa.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/NAM/1-e7b3a0bd3e138a8d3423ddb036387da5.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

2 × four =