Sefania 3

Hatima Ya Yerusalemu

1 Ole wa mji wa wadhalimu,

waasi na waliotiwa unajisi!

2 Hautii mtu ye yote,

haukubali maonyo.

HaumtumainiBwana,

haukaribii karibu na Mungu wake.

3 Maafisa wake ni simba wangurumao,

watawala wake ni mbwa mwitu wa jioni,

ambao hawabakizi cho chote

kwa ajili ya asubuhi.

4 Manabii wake ni wenye kiburi,

ni wadanganyifu.

Makuhani wake hunajisi patakatifu

na kuihalifu sheria.

5 Bwanaaliye ndani yake ni mwenye haki,

hafanyi kosa.

Asubuhi kwa asubuhi hutoa haki yake,

kila kukipambazuka huitimiza,

bali mtu dhalimu hana aibu.

6 “Nimeyafutilia mbali mataifa,

ngome zao zimebomolewa.

Nimeziacha barabara ukiwa,

hakuna anayepita humo.

Miji yao imeharibiwa;

hakuna mmoja atakayeachwa:

hakuna hata mmoja.

7 Niliuambia huo mji,

‘Hakika utaniogopa na kukubali maonyo!’

Ndipo makao yake hayatafutiliwa mbali,

wala adhabu zangu zote hazitakuja juu yake.

Lakini walikuwa bado na shauku

kutenda kwa upotovu katika yote waliyofanya.”

8 Bwanaanasema,

“Kwa hiyo ningojee mimi,

siku nitakayosimama kuteka nyara.

Nimeamua kukusanya mataifa,

kukusanya falme

na kumimina ghadhabu yangu juu yao,

hasira yangu kali yote.

Dunia yote itateketezwa

kwa moto wa wivu wa hasira yangu.

9 “Ndipo nitatakasa midomo ya mataifa,

kwamba wote waweze kuliitia jina laBwana

na kumtumikia kwa pamoja.

10 Kutoka ng’ambo ya mito ya Kushi

watu wangu wanaoniabudu,

watu wangu waliotawanyika,

wataniletea sadaka.

11 Siku hiyo hutaaibishwa

kwa ajili ya makosa yote ulionitendea,

kwa sababu nitawaondoa kutoka mji huu

wale wote wanaoshangilia

katika kiburi chao.

Kamwe hutajivuna tena

katika kilima changu kitakatifu.

12 Lakini nitakuachia ndani yako

wapole na wanyenyekevu,

ambao wanatumaini jina laBwana.

13 Mabaki ya Israeli hayatafanya kosa;

hawatasema uongo,

wala udanganyifu hautakuwa

katika vinywa vyao.

Watakula na kulala

wala hakuna ye yote

atakayewaogopesha.”

14 Imba, Ee Binti Sayuni;

paza sauti, Ee Israeli!

Furahi na kushangilia kwa moyo wako wote,

Ee Binti Yerusalemu!

15 Bwanaamekuondolea adhabu yako,

amewarudisha nyuma adui zako.

Bwana, Mfalme wa Israeli, yu pamoja nawe;

kamwe hutaogopa tena madhara yo yote.

16 Katika siku hiyo watauambia Yerusalemu,

“Usiogope, Ee Sayuni;

usiiache mikono yako ilegee.

17 BwanaMungu wako yu pamoja nawe,

yeye ni mwenye nguvu kuokoa.

Atakufurahia kwa furaha kubwa,

atakutuliza kwa pendo lake,

atakufurahia kwa kuimba.”

18 “Huzuni katika sikukuu zilizoamriwa

nitaziondoa kwenu;

hizo ni mzigo wa fedheha kwenu.

19 Katika wakati huo nitawashughulikia

wote waliokudhulumu;

nitaokoa kilema na kukusanya

wale ambao wametawanywa.

Nitawapa sifa na heshima

katika kila nchi ambamo waliaibishwa.

20 Wakati huo nitawakusanya;

wakati huo nitawaleta nyumbani.

Nitawapa sifa na heshima

miongoni mwa mataifa yote ya dunia

wakati nitakapowarudishia mateka yenu

mbele ya macho yenu hasa,”

asemaBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/ZEP/3-f093c4ce0bcf69b438670c034e31a7bd.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

4 × 4 =