Yeremia 17

Dhambi Ya Yuda Na Adhabu yake

1 “Dhambi ya Yuda imechorwa kwa kalamu ya chuma,

imeandikwa kwa ncha ya almasi,

kwenye vibao vya mioyo yao

na kwenye pembe za madhabahu zao.

2 Hata watoto wao wanakumbuka madhabahu zao

# na nguzo za Ashera

kandokando ya miti iliyotanda

na juu ya vilima virefu.

3 Mlima wangu katika nchi pamoja na utajiri

na hazina zako zote

nitazitoa ziwe nyara,

pamoja na mahali pako pa juu pa kuabudia miungu

kwa sababu ya dhambi katika nchi yako yote.

4 Kwa kosa lako mwenyewe utaupoteza

urithi niliokupa.

Nitakufanya mtumwa wa adui zako

katika nchi usiyoijua,

kwa kuwa umeiwasha hasira yangu,

nayo itawaka milele.”

5 Hili ndilo asemaloBwana:

“Amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu,

ategemeaye mwenye mwili

kwa ajili ya nguvu zake,

ambaye moyo wake

umemwachaBwana.

6 Atakuwa kama kichaka cha jangwani;

hataona mafanikio yatakapokuja.

Ataishi katika sehemu zisizo na maji,

katika nchi ya chumvi ambapo

hakuna ye yote aishiye humo.

7 “Lakini amebarikiwa mtu ambaye tumaini lake ni katikaBwana,

ambaye matumaini yake ni katikaBwana.

8 Atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji

uenezao mizizi yake

karibu na kijito cha maji.

Hauogopi wakati wa joto ujapo;

majani yake ni mabichi daima.

Hauna hofu katika mwaka wa ukame

na hautaacha kuzaa matunda.”

9 Moyo ni mdanganyifu kuliko vitu vyote,

ni mwovu kupita kiasi.

Ni nani awezaye kuujua?

10 “MimiBwanahuchunguza moyo

na kuzijaribu nia,

kumlipa mtu kwa kadiri ya mwenendo wake,

kwa kadiri ya matendo yake yanavyostahili.”

11 Kama kware aanguaye mayai asiyoyataga,

ndivyo alivyo mtu apataye mali

kwa njia zisizo za haki.

Maisha yake yafikapo katikati, siku zitamwacha,

na mwishoni atabainika kuwa mpumbavu.

12 Kiti cha enzi kilichotukuzwa, kilichoinuliwa tangu mwanzo,

ndiyo sehemu yetu ya mahali patakatifu.

13 EeBwana, uliye tumaini la Israeli,

wote wakuachao wataaibika.

Wale wanaogeukia mbali nawe wataandikwa mavumbini

kwa sababu wamemwachaBwana,

chemchemi ya maji yaliyo hai.

14 Uniponye, EeBwana, nami nitaponyeka;

uniokoe nami nitaokoka,

kwa maana wewe ndiwe ninayekusifu.

15 Wao huendelea kuniambia,

“Liko wapi neno laBwana?

Sasa na litimie!”

16 Sijakukimbia na kuacha kuwa mchungaji wako;

unajua sijaitamani siku ya kukata tamaa.

Kile kipitacho midomoni mwangu

ki wazi mbele yako.

17 Usiwe kwangu kitu cha kunitia hofu kuu;

wewe ndiwe kimbilio langu katika siku ya maafa.

18 Watesi wangu na waaibishwe,

lakini nilinde mimi nisiaibike;

wao na watiwe hofu kuu,

lakini unilinde mimi na hofu kuu.

Uwaletee siku ya maafa;

waangamize kwa maangamizi maradufu.

Kuiadhimisha Sabato

19 Hili ndiloBwanaaliloniambia: “Nenda ukasimame kwenye lango la watu, mahali ambako wafalme wa Yuda huingilia na kutokea, simama pia kwenye malango mengine yote ya Yerusalemu.

20 Waambie, ‘Sikieni neno laBwana, Enyi wafalme wa Yuda nanyi watu wote wa Yuda na kila mmoja aishiye Yerusalemu apitaye katika malango haya.

21 Hili ndilo asemaloBwana: Jihadharini msije mkabeba mzigo siku ya Sabato, wala kuingiza mzigo kupitia malango ya Yerusalemu.

22 Msitoe mizigo nje ya nyumba zenu wala kufanya kazi yo yote wakati wa Sabato, lakini itakaseni siku ya Sabato, kama nilivyowaamuru baba zenu.

23 Hata hivyo hawakusikiliza wala kujali, walishupaza shingo zao na hawakutaka kusikia wala kukubali marudi.

24 Lakini mkiwa waangalifu katika kunitii, asemaBwana, nanyi msipoleta mzigo wo wote kupitia malango ya mji huu wakati wa Sabato, lakini mkaitakasa siku ya Sabato kwa kutofanya kazi siku hiyo,

25 ndipo wafalme wakaao juu ya kiti cha enzi cha Daudi, wataingia kupitia malango ya mji huu pamoja na maafisa wao. Wao na maafisa wao watakuja wakiwa wamepanda magari na farasi, wakiandamana na watu wa Yuda na wale waishio Yerusalemu, nao mji huu utakaliwa na watu daima.

26 Watu watakuja kutoka miji ya Yuda na vijiji vinavyoizunguka Yerusalemu, kutoka nchi ya Benyamini na chini ya vilima vya magharibi, kutoka nchi ya vilima na Negebu, wakileta sadaka za kuteketezwa na dhabihu, sadaka za nafaka, uvumba na sadaka za shukrani kwenye nyumba yaBwana.

27 Lakini ikiwa hamtanitii mimi kwa kuitakasa Sabato na kwa kutochukua mzigo wo wote mnapoingia katika malango ya Yerusalemu wakati wa Sabato, basi nitawasha moto usiozimika katika malango ya Yerusalemu utakaoteketeza ngome zake.’ ”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/17-f25fcda9b39efdb8a11607a42c6053f0.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

14 + nine =