Yeremia 19

Gudulia La Udongo Lililovunjika

1 Hili ndilo asemaloBwana: “Nenda ukanunue gudulia la udongo kutoka kwa mfinyanzi. Wachukue baadhi ya wazee wa watu na wa makuhani

2 na mtoke mwende mpaka kwenye Bonde la Ben-Hinomu, karibu na ingilio la Lango la Vigae. Huko tangaza maneno ninayokuambia,

3 nawe useme, ‘Sikieni neno laBwana, enyi wafalme wa Yuda na watu wa Yerusalemu. Hili ndiloBwanaMwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli asemalo: Sikilizeni! Nitaleta maafa mahali hapa ambayo yatafanya masikio ya kila mmoja atakayesikia habari zake yawashe.

4 Kwa kuwa wameniacha na kupafanya mahali hapa kuwa pa miungu ya kigeni, wameiteketezea sadaka miungu ambayo wao wala baba zao wala wafalme wa Yuda kamwe hawakuijua, nao wamelijaza eneo hili kwa damu isiyo na hatia.

5 Wamejenga mahali pa juu pa kuabudia miungu pa Baali ili kuteketeza wana wao katika moto kama sadaka kwa Baali, kitu ambacho sikukiamuru wala kukitaja, wala hakikuingia akilini mwangu.

6 Hivyo jihadharini, siku zinakuja, asemaBwana, wakati watu hawatapaita tena mahali hapa Tofethi ama Bonde la Ben-Hinomu, bali Bonde la Machinjo.

7 “ ‘Nitaiharibu mipango ya Yuda na Yerusalemu mahali hapa. Nitawafanya waanguke kwa upanga mbele ya adui zao, katika mikono ya wale watafutao uhai wao, nami nitaitoa mizoga yao kuwa chakula cha ndege wa angani na wanyama wa nchi.

8 Nitauharibu mji huu na kuufanya kitu cha kudharauliwa, wote wapitao karibu watashangaa na wataudhihaki kwa ajili ya majeraha yake yote.

9 Nitawafanya wao kula nyama ya wana wao na binti zao, kila mmoja atakula nyama ya mwenzake wakati wa dhiki ya kuzungukwa na jeshi lililowekwa juu yao na adui wanaotafuta uhai wao.’

10 “Kisha livunje lile gudulia wakati wale walio pamoja nawe wakiwa wanaangalia,

11 uwaambie, ‘Hili ndiloBwanaMwenye Nguvu Zote asemalo: Nitalivunja taifa hili na mji huu kama gudulia hili la mfinyanzi lilivyovunjwa, nalo haliwezi kutengenezeka tena. Watawazika waliokufa huko Tofethi hata isiwepo nafasi zaidi.

12 Hivi ndivyo nitakavyopafanya mahali hapa na kwa wale waishio ndani yake, asemaBwana. Nitaufanya mji huu kama Tofethi.

13 Nyumba zilizoko Yerusalemu na zile za wafalme wa Yuda zitatiwa unajisi kama mahali hapa, yaani, Tofethi. Nyumba zote ambazo walifukiza uvumba juu ya mapaa yake kwa jeshi lote la angani na kumimina dhabihu ya kinywaji kwa miungu mingine.’ ”

14 Kisha Yeremia akarudi kutoka Tofethi, mahali ambapoBwanaalikuwa amemtuma kutoa unabii, akasimama katika ua wa Hekalu laBwanana kuwaambia watu wote,

15 “Hili ndiloBwanaMwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, asemalo: ‘Sikilizeni! Nitaleta juu ya mji huu pamoja na vijiji vinavyouzunguka kila maafa niliyosema dhidi yake, kwa sababu wamekuwa na shingo ngumu na hawakuyasikiliza maneno yangu.’ ”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/19-314cbf23476c1ea047aacb146d7dd69e.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

10 − 8 =