Yeremia 4

1 “Ikiwa utataka kurudi, Ee Israeli,

nirudie mimi,”

asemaBwana.

“Ikiwa utataka kuachilia mbali na macho yangu

sanamu zako za kuchukiza

na usiendelee kutangatanga,

2 ikiwa kwa kweli, kwa haki na kwa unyofu utaapa,

‘Kwa hakika kama vileBwanaaishivyo,’

ndipo mataifa yatakapobarikiwa naye

na katika yeye watajitukuza.”

3 Hili ndilo asemaloBwanakwa watu wa Yuda na kwa Yerusalemu:

“Vunjeni mabonge ya udongo

kwenye mashamba yenu yasiyolimwa

wala msipande katikati ya miiba.

4 Jitahirini katikaBwana,

tahirini mioyo yenu,

enyi wanaume wa Yuda

na watu wa Yerusalemu,

la sivyo ghadhabu yangu itatoka kwa nguvu

na kuwaka kama moto

kwa sababu ya uovu mliotenda,

ikiwaka pasipo wa kuizima.

Maafa Kutoka Kaskazini

5 “Tangaza katika Yuda na upige mbiu katika Yerusalemu na kusema:

‘Piga tarumbeta katika nchi yote!’

Piga kelele na kusema:

‘Kusanyikeni pamoja!

Tukimbilie katika miji yenye maboma!’

6 Onyesheni ishara ili kwenda Sayuni!

Kimbilieni kwenye usalama pasipo kuchelewa!

Kwa kuwa ninaleta maafa kutoka kaskazini,

yaani maangamizi ya kutisha.”

7 Simba ametoka nje ya pango lake,

mharabu wa mataifa amejipanga.

Ametoka mahali pake

ili kuja kuangamiza nchi yenu.

Miji yenu itakuwa magofu

pasipo mtu wa kuishi humo.

8 Hivyo vaeni nguo za magunia,

ombolezeni na kulia kwa huzuni,

kwa kuwa hasira kali yaBwana

haijaondolewa kwetu.

9 “Katika siku ile,” asemaBwana

“mfalme na maafisa watakata tamaa,

makuhani watafadhaika,

na manabii watashangazwa mno.”

10 Ndipo niliposema, “Aa,BwanaMwenyezi, umewadanganyaje kabisa watu hawa na Yerusalemu kwa kusema, ‘Mtakuwa na amani,’ wakati upanga uko kwenye makoo yetu!”

11 Wakati huo watu hawa na Yerusalemu wataambiwa, “Upepo wa moto kutoka miinuko iliyo kame katika jangwa unavuma kuelekea watu wangu, lakini sio kupepeta au kutakasa,

12 upepo wenye nguvu sana kuliko wa kupepeta na kutakasa utakuja kwa amri yangu. Sasa natangaza hukumu zangu dhidi yao.”

13 Tazama! Anakuja kama mawingu,

magari yake yanakuja

kama upepo wa kisulisuli,

farasi wake ni wenye mbio kuliko tai.

Ole wetu! Tunaangamia!

14 Ee Yerusalemu, uusafishe uovu

kutoka moyoni mwako na uokolewe.

Utaendelea kuficha mawazo mapotovu

mpaka lini?

15 Sauti inatangaza kutoka Dani,

ikipiga mbiu ya maafa kutoka vilima vya Efraimu.

16 “Waambie mataifa jambo hili,

piga mbiu hii dhidi ya Yerusalemu:

‘Jeshi la kuzingira linakuja kutoka nchi ya mbali,

likipiga kelele ya vita dhidi ya miji ya Yuda.

17 Wamemzunguka kama watu walindao shamba,

kwa sababu amefanya uasi dhidi yangu,’ ”

asemaBwana.

18 “Mwenendo wako na matendo yako mwenyewe

yameleta haya juu yako.

Hii ndiyo adhabu yako.

Tazama jinsi ilivyo chungu!

Tazama jinsi inavyochoma moyo!”

19 Ee mtima wangu, mtima wangu!

Ninagaagaa kwa maumivu.

Ee maumivu makuu ya moyo wangu!

Moyo wangu umefadhaika ndani yangu,

siwezi kunyamaza.

Kwa sababu nimesikia sauti ya tarumbeta,

nimesikia kelele ya vita.

20 Maafa baada ya maafa,

nchi yote imekuwa magofu.

Kwa ghafula mahema yangu yameangamizwa,

makazi yangu kwa muda mfupi.

21 Hata lini nitaendelea kuona bendera ya vita

na kusikia sauti za tarumbeta?

22 “Watu wangu ni wapumbavu,

hawanijui mimi.

Ni watoto wasio na akili,

hawana ufahamu.

Ni hodari kutenda mabaya,

hawajui kutenda yaliyo mema.”

23 Niliitazama dunia,

nayo haikuwa na umbo tena ni tupu;

niliziangalia mbingu,

mianga ilikuwa imetoweka.

24 Niliitazama milima,

nayo ilikuwa ikitetemeka,

vilima vyote vilikuwa vikiyumbayumba.

25 Nilitazama, wala watu hawakuwepo;

kila ndege wa angani alikuwa ameruka zake.

26 Nilitazama, hata nchi iliyokuwa imestawi vizuri

imekuwa jangwa,

miji yake yote ilikuwa magofu mbele zaBwana,

mbele ya hasira yake kali.

27 Hivi ndivyoBwanaasemavyo:

“Nchi yote itaharibiwa,

ingawa sitaiangamiza kabisa.

28 Kwa hiyo dunia itaomboleza

na mbingu zilizo juu zitakuwa giza,

kwa sababu nimesema nami sitakuwa na huruma,

nimeamua na wala sitageuka.”

29 Kwa sauti ya wapanda farasi na wapiga upinde

kila mji unakimbia.

Baadhi wanakimbilia vichakani,

baadhi wanapanda juu ya miamba.

Miji yote imeachwa,

hakuna aishiye ndani yake.

30 Unafanya nini, ewe uliyeharibiwa?

Kwa nini unajivika vazi jekundu

na kuvaa vito vya dhahabu?

Kwa nini unapaka macho yako rangi?

Unajipamba bure.

Wapenzi wako wanakudharau,

wanautafuta uhai wako.

31 Nasikia kilio kama cha mwanamke

aliye katika utungu wa kuzaa,

kilio cha uchungu kama cha anayemzaa

mtoto wake wa kwanza:

kilio cha Binti Sayuni akitapatapa ili aweze kupumua,

akiinua mikono yake, akisema,

“Ole wangu! Ninazimia;

maisha yangu yamekabidhiwa kwa wauaji.”

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/4-d6b16d9a29c1139a2216bc13a082d78a.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

1 × 3 =