Yeremia 5

Hakuna Hata Mmoja Aliye Mkamilifu

1 “Pandeni na kushuka katika mitaa ya Yerusalemu,

tazameni pande zote na mkumbuke,

tafuteni katika viwanja vyake.

Kama mtaweza kumpata hata mtu mmoja tu

atendaye kwa uaminifu na kutafuta kweli,

nitausamehe mji huu.

2 Ingawa wanasema, ‘Kwa hakika kamaBwanaaishivyo,’

bado wanaapa kwa uongo.”

3 EeBwana, je, macho yako hayaitafuti kweli?

Uliwapiga, lakini hawakusikia maumivu,

uliwapondaponda lakini walikataa marudi.

Walifanya nyuso zao kuwa ngumu kuliko jiwe

nao walikataa kutubu.

4 Ndipo nikasema, “Hawa ni maskini tu;

wao ni wapumbavu,

kwa maana hawaijui njia yaBwana,

sheria ya Mungu wao.

5 Kwa hiyo nitakwenda kwa viongozi

na kuzungumza nao,

hakika wao wanaijua njia yaBwana,

sheria ya Mungu wao.”

Lakini kwa nia moja nao pia walikuwa wameivunja nira

na kuvivunja vifungo.

6 Kwa hiyo simba kutoka mwituni atawashambulia,

mbwa mwitu kutoka jangwani atawaangamiza,

chui atawavizia karibu na miji yao

kumrarua vipande vipande ye yote

atakayethubutu kutoka nje,

kwa maana maasi yao ni makubwa

na kukengeuka kwao kumekuwa ni kwingi.

7 “Kwa nini niwasamehe?

Watoto wenu wameniacha

na kuapa kwa miungu ambayo si miungu.

Niliwapatia mahitaji yao yote,

lakini bado wamefanya uzinzi

na kusongana katika nyumba za makahaba.

8 Wamelishwa vizuri, kama farasi waume wenye tamaa nyingi,

kila mmoja akimlilia

mke wa mwanaume mwingine.

9 Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya hili?”

asemaBwana.

“Je, nisijilipizie kisasi

juu ya taifa kama hili?

10 “Piteni katika mashamba yake ya mizabibu na kuyaharibu,

lakini msiangamize kabisa.

Pogoeni matawi yake,

kwa kuwa watu hawa sio waBwana.

11 Nyumba ya Israeli na nyumba ya Yuda

wamekuwa si waaminifu kwangu kamwe,”

asemaBwana.

12 Wamedanganya kuhusuBwana,

wamesema, “Yeye hatafanya jambo lo lote!

Hakuna dhara litakalotupata;

kamwe hatutaona upanga wala njaa.

13 Manabii ni upepo tu, wala neno halimo ndani yao,

kwa hiyo hayo wayasemayo

na yatendeke kwao.”

14 Kwa hiyo hili ndilo asemaloBwanaMungu Mwenye Nguvu Zote:

“Kwa sababu watu hawa wamesema maneno haya,

nitayafanya maneno yangu

vinywani mwenu kuwa moto

na watu hawa wawe kuni

zinazoliwa na huo moto.

15 Ee nyumba ya Israeli,” asemaBwana,

“Ninaleta taifa toka mbali dhidi yako,

taifa la kale na linaloendelea kudumu,

taifa ambalo lugha yao huijui,

wala msemo wao huwezi kuuelewa.

16 Podo zao ni kama kaburi lililo wazi,

wote ni mashujaa hodari wa vita.

17 Watayaangamiza mazao yenu na chakula chenu,

wataangamiza wana wenu na mabinti zenu;

wataangamiza makundi yenu

ya kondoo na mbuzi, na ya ng’ombe,

wataangamiza mizabibu yenu na mitini yenu.

Kwa upanga wataangamiza

miji yenye maboma mliyoitumainia.

18 “Hata hivyo katika siku hizo, sitakuangamiza kabisa,” asemaBwana.

19 “Nao watu watakapouliza, ‘Kwa niniBwana, Mungu wetu ametufanyia mambo haya yote?’ Utawaambia, ‘Kama vile mlivyoniacha mimi na kutumikia miungu migeni katika nchi yenu wenyewe, ndivyo sasa mtakavyowatumikia wageni katika nchi ambayo si yenu.’

20 “Itangazie nyumba ya Yakobo hili

na ulipigie mbiu katika Yuda:

21 Sikieni hili, enyi wapumbavu na watu msio na akili,

mlio na macho lakini hamwoni,

mlio na masikio lakini hamsikii:

22 Je, haiwapasi kuniogopa mimi?” asemaBwana.

“Je, haiwapasi kutetemeka mbele zangu?

Niliufanya mchanga kuwa mpaka wa bahari,

kizuizi cha milele ambacho haiwezi kupita.

Mawimbi yanaweza kuumuka, lakini hayawezi kuupita;

yanaweza kunguruma, lakini hayawezi kuuvuka.

23 Lakini watu hawa wana mioyo ya ukaidi na ya uasi,

wamegeukia mbali na kwenda zao.

24 Wao hawaambiani wenyewe,

‘Sisi na tumwogopeBwanaMungu wetu,

anayetupatia mvua za masika na za vuli

kwa majira yake,

anayetuhakikishia majuma ya mavuno

kwa utaratibu.’

25 Matendo yenu mabaya yamezuia haya yote,

dhambi zenu zimewafanya msipate mema.

26 “Miongoni mwa watu wangu wamo walio waovu

wanaovizia kama watu wanaotega ndege

na kama wale wanaoweka mitego

kuwakamata watu.

27 Kama vitundu vilivyojaa ndege,

nyumba zao zimejaa udanganyifu;

wamekuwa matajiri na wenye nguvu,

28 wamenenepa na kunawiri.

Matendo yao maovu hayana kikomo;

hawatetei mashauri ya yatima

wapate kushinda,

hawatetei haki za maskini.

29 Je, nisiwaadhibu kwa ajili ya hili?”

asemaBwana.

“Je, nisijilipizie kisasi

juu ya taifa kama hili?

30 “Jambo la kutisha na kushtusha

limetokea katika nchi hii:

31 Manabii wanatabiri uongo,

makuhani wanatawala

kwa mamlaka yao wenyewe,

nao watu wangu wanapenda hivyo.

Lakini mtafanya nini mwisho wake?

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/JER/5-db89a177e08909e60b4f558336801058.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

fourteen + 5 =