Sala Ya Kuomba Msaada
(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)
1 Mpaka lini, EeBwana? Je, utanisahau milele?
Utanificha uso wako mpaka lini?
2 Nitapambana na mawazo yangu mpaka lini
na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu?
Adui zangu watanishinda mpaka lini?
3 Nitazame unijibu, EeBwanaMungu wangu.
Uyatie nuru macho yangu,
ama sivyo nitalala usingizi wa mauti;
4 adui yangu atasema, “Nimemshinda,”
nao adui zangu watashangilia nitakapoanguka.
5 Lakini ninategemea upendo wako usiokoma;
moyo wangu unashangilia katika wokovu wako.
6 NitamwimbiaBwana,
kwa kuwa amekuwa mwema kwangu.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/13-e4324ab50d31ef0ba6d185a93f9159ae.mp3?version_id=1627—