Zaburi 13

Sala Ya Kuomba Msaada

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)

1 Mpaka lini, EeBwana? Je, utanisahau milele?

Utanificha uso wako mpaka lini?

2 Nitapambana na mawazo yangu mpaka lini

na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu?

Adui zangu watanishinda mpaka lini?

3 Nitazame unijibu, EeBwanaMungu wangu.

Uyatie nuru macho yangu,

ama sivyo nitalala usingizi wa mauti;

4 adui yangu atasema, “Nimemshinda,”

nao adui zangu watashangilia nitakapoanguka.

5 Lakini ninategemea upendo wako usiokoma;

moyo wangu unashangilia katika wokovu wako.

6 NitamwimbiaBwana,

kwa kuwa amekuwa mwema kwangu.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/13-e4324ab50d31ef0ba6d185a93f9159ae.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

seventeen − 10 =