Uovu Wa Wanadamu
(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Mahalathi. Zaburi Ya Daudi)
1 Mpumbavu anasema moyoni mwake,
“Hakuna Mungu.”
Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa;
hakuna atendaye mema.
2 Toka mbinguniBwanaanawachungulia
wanadamu chini
aone kama wako wenye akili,
wo wote wanaomtafuta Mungu.
3 Wote wamepotoka,
wameoza wote pamoja;
hakuna atendaye mema,
naam! Hata mmoja.
4 Je, watendao mabaya hawatajifunza:
wale ambao huwala watu wangu
kama watu walavyo mkate,
hao ambao hawamwitiBwana?
5 Hapo ndipo walipo, wameingiwa na hofu nyingi,
maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.
6 Ninyi watenda mabaya mnakwamisha mipango ya maskini,
baliBwanani kimbilio lao.
7 Laiti wokovu wa Israeli
ungalikuja kutoka Sayuni!
WakatiBwanaarejeshapo
wafungwa wa watu wake,
Yakobo na ashangilie,
Israeli na afurahi!
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/14-dc78f06060b2adf0d54a4e409f70b76f.mp3?version_id=1627—