Zaburi 14

Uovu Wa Wanadamu

(Kwa Mwimbishaji: Mtindo Wa Mahalathi. Zaburi Ya Daudi)

1 Mpumbavu anasema moyoni mwake,

“Hakuna Mungu.”

Wameharibika, matendo yao ni maovu kabisa;

hakuna atendaye mema.

2 Toka mbinguniBwanaanawachungulia

wanadamu chini

aone kama wako wenye akili,

wo wote wanaomtafuta Mungu.

3 Wote wamepotoka,

wameoza wote pamoja;

hakuna atendaye mema,

naam! Hata mmoja.

4 Je, watendao mabaya hawatajifunza:

wale ambao huwala watu wangu

kama watu walavyo mkate,

hao ambao hawamwitiBwana?

5 Hapo ndipo walipo, wameingiwa na hofu nyingi,

maana Mungu yupo pamoja na wenye haki.

6 Ninyi watenda mabaya mnakwamisha mipango ya maskini,

baliBwanani kimbilio lao.

7 Laiti wokovu wa Israeli

ungalikuja kutoka Sayuni!

WakatiBwanaarejeshapo

wafungwa wa watu wake,

Yakobo na ashangilie,

Israeli na afurahi!

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/14-dc78f06060b2adf0d54a4e409f70b76f.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

2 × 1 =