Zaburi 143

Maombi Ya Kuokolewa Dhidi Ya Adui

(Zaburi Ya Daudi)

1 EeBwana, sikia sala yangu,

sikiliza kilio changu unihurumie;

katika uaminifu na haki yako

njoo unisaidie.

2 Usimhukumu mtumishi wako,

kwa kuwa hakuna mtu anayeishi

mwenye haki mbele zako.

3 Adui hunifuatilia,

hunipondaponda chini;

hunifanya niishi gizani

kama wale waliokufa zamani.

4 Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu,

moyo wangu ndani yangu unakata tamaa.

5 Nakumbuka siku za zamani;

natafakari juu ya kazi zako zote,

naangalia juu ya kazi ambazo

mikono yako imezifanya.

6 Nanyosha mikono yangu kwako,

nafsi yangu inakuonea kiu

kama ardhi kame.

7 EeBwana, unijibu haraka,

roho yangu inazimia.

Usinifiche uso wako,

ama sivyo nitafanana

na wale washukao shimoni.

8 Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma,

kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako.

Nionyeshe njia nitakayoiendea,

kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu.

9 EeBwana, uniokoe na adui zangu,

kwa kuwa nimejificha kwako.

10 Nifundishe kufanya mapenzi yako,

kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu,

Roho wako mwema na aniongoze

katika nchi tambarare.

11 EeBwana, kwa ajili ya jina lako,

hifadhi maisha yangu,

kwa haki yako nitoe katika taabu.

12 Kwa upendo wako usiokoma,

nyamazisha adui zangu;

waangamize watesi wangu wote,

kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/143-cd2153934e693222771bbe87b6f52c43.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

16 − 11 =