Zaburi 146

Kumsifu Mungu Mwokozi

1 MsifuniBwana!

Ee nafsi yangu, umsifuBwana,

2 NitamsifuBwanamaisha yangu yote;

nitamwimbia Mungu wangu sifa

wakati wote niishipo.

3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu,

kwa wanadamu ambao hufa,

ambao hawawezi kuokoa.

4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini,

siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.

5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo

ni msaada wake,

ambaye tumaini lake

ni katikaBwana, Mungu wake,

6 Muumba wa mbingu na dunia,

bahari na vyote vilivyomo ndani yake:

Bwanaanayedumu kuwa mwaminifu

milele na milele.

7 Naye huwapatia haki walioonewa

na kuwapa wenye njaa chakula.

Bwanahuwaweka wafungwa huru,

8 Bwanahuwafumbua vipofu macho,

Bwanahuwainua waliolemewa na mizigo yao,

Bwanahuwapenda wenye haki.

9 Bwanahuwalinda wageni

na kuwategemeza yatima na wajane,

lakini hupinga njia za waovu.

10 Bwanaatamiliki milele,

Mungu wako, Ee Sayuni,

kwa vizazi vyote.

MsifuniBwana.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/146-95c39d5fcce9e781a19eaaf806aab6ef.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

ten − 4 =