Kumsifu Mungu Mwokozi
1 MsifuniBwana!
Ee nafsi yangu, umsifuBwana,
2 NitamsifuBwanamaisha yangu yote;
nitamwimbia Mungu wangu sifa
wakati wote niishipo.
3 Usiweke tumaini lako kwa wakuu,
kwa wanadamu ambao hufa,
ambao hawawezi kuokoa.
4 Roho yao itokapo hurudi mavumbini,
siku hiyo hiyo mipango yao yote hukoma.
5 Heri yeye ambaye Mungu wa Yakobo
ni msaada wake,
ambaye tumaini lake
ni katikaBwana, Mungu wake,
6 Muumba wa mbingu na dunia,
bahari na vyote vilivyomo ndani yake:
Bwanaanayedumu kuwa mwaminifu
milele na milele.
7 Naye huwapatia haki walioonewa
na kuwapa wenye njaa chakula.
Bwanahuwaweka wafungwa huru,
8 Bwanahuwafumbua vipofu macho,
Bwanahuwainua waliolemewa na mizigo yao,
Bwanahuwapenda wenye haki.
9 Bwanahuwalinda wageni
na kuwategemeza yatima na wajane,
lakini hupinga njia za waovu.
10 Bwanaatamiliki milele,
Mungu wako, Ee Sayuni,
kwa vizazi vyote.
MsifuniBwana.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/146-95c39d5fcce9e781a19eaaf806aab6ef.mp3?version_id=1627—