Maombi Kwa Ajili Ya Ushindi
(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)
1 Bwanana akujibu unapokuwa katika dhiki,
jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako.
2 Na akutumie msaada kutoka patakatifu
na akupatie msaada kutoka Sayuni.
3 Na azikumbuke dhabihu zako zote
na azikubali sadaka zako za kuteketezwa.
4 Na akujalie haja ya moyo wako
na aifanikishe mipango yako yote.
5 Tutashangilia kwa furaha utakaposhinda,
tutainua bendera zetu kwa jina la Mungu wetu.
Bwanana akupe haja zako zote.
6 Sasa nafahamu kuwaBwana
humwokoa mpakwa mafuta wake,
humjibu kutoka mbingu yake takatifu
kwa nguvu za wokovu wa mkono wake wa kuume.
7 Wengine wanatumaini magari ya vita na wengine farasi,
bali sisi tutalitumainia jina laBwana, Mungu wetu.
8 Wao wameshushwa chini na kuanguka,
bali sisi tunainuka
na kusimama imara.
9 EeBwana, mwokoe mfalme!
Utujibu wakati tunapokuita!
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/20-577ad76d017b4bd9d7e850b41c9fe1d4.mp3?version_id=1627—