Zaburi 20

Maombi Kwa Ajili Ya Ushindi

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)

1 Bwanana akujibu unapokuwa katika dhiki,

jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako.

2 Na akutumie msaada kutoka patakatifu

na akupatie msaada kutoka Sayuni.

3 Na azikumbuke dhabihu zako zote

na azikubali sadaka zako za kuteketezwa.

4 Na akujalie haja ya moyo wako

na aifanikishe mipango yako yote.

5 Tutashangilia kwa furaha utakaposhinda,

tutainua bendera zetu kwa jina la Mungu wetu.

Bwanana akupe haja zako zote.

6 Sasa nafahamu kuwaBwana

humwokoa mpakwa mafuta wake,

humjibu kutoka mbingu yake takatifu

kwa nguvu za wokovu wa mkono wake wa kuume.

7 Wengine wanatumaini magari ya vita na wengine farasi,

bali sisi tutalitumainia jina laBwana, Mungu wetu.

8 Wao wameshushwa chini na kuanguka,

bali sisi tunainuka

na kusimama imara.

9 EeBwana, mwokoe mfalme!

Utujibu wakati tunapokuita!

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/20-577ad76d017b4bd9d7e850b41c9fe1d4.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

7 − 5 =