Zaburi 23

Bwana Mchungaji Wetu

(Zaburi Ya Daudi)

1 Bwanandiye mchungaji wangu,

sitapungukiwa na kitu.

2 Hunilaza katika malisho

ya majani mabichi,

kando ya maji matulivu huniongoza,

3 huifanya upya nafsi yangu.

Huniongoza katika njia za haki

kwa ajili ya jina lake.

4 Hata kama nikipita katikati

ya bonde la uvuli wa mauti,

sitaogopa mabaya,

kwa maana wewe upo pamoja nami;

fimbo yako na mkongojo wako

vyanifariji.

5 Waandaa meza mbele yangu

machoni pa adui zangu.

Umenipaka mafuta kichwani pangu,

kikombe changu kinafurika.

6 Hakika wema na upendo vitanifuata

siku zote za maisha yangu,

nami nitakaa nyumbani mwaBwana

milele.

—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/23-dc391d02f87b42fe58b081c51d280890.mp3?version_id=1627—

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *

three × 4 =