Mfalme Mkuu
(Zaburi Ya Daudi)
1 Dunia ni mali yaBwana, pamoja na vyote vilivyomo ndani yake,
ulimwengu na wote waishio ndani yake,
2 maana aliiwekea misingi yake baharini
na kuifanya imara juu ya maji.
3 Nani awezaye kuupanda mlima waBwana?
Ni nani awezaye kusimama patakatifu pake?
4 Ni yule mwenye mikono safi na moyo mweupe,
yule ambaye hakuinulia sanamu nafsi yake
au kuapa kwa kitu cha uongo.
5 Huyo atapokea baraka kutoka kwaBwana,
na hukumu ya haki
kutoka kwa Mungu Mwokozi wake.
6 Hiki ndicho kizazi cha wale wamtafutao,
wale wautafutao uso wako,
Ee Mungu wa Yakobo.
7 Inueni vichwa vyenu, enyi malango,
inukeni enyi milango ya kale,
ili mfalme wa utukufu apate kuingia.
8 Ni nani huyu Mfalme wa utukufu?
NiBwanaaliye na nguvu na uweza,
niBwanaaliye hodari katika vita.
9 Inueni vichwa vyenu, enyi malango,
viinueni juu enyi milango ya kale,
ili mfalme wa utukufu apate kuingia.
10 Ni nani huyu, huyu mfalme wa utukufu?
NiBwanaMwenye Nguvu Zote;
yeye ndiye Mfalme wa utukufu.
—https://d1b84921e69nmq.cloudfront.net/337/32k/PSA/24-91c40c17d34778b02a40e9bd38202f5a.mp3?version_id=1627—