Yuda Na Benyamini Zajengwa Ngome 1 Ikawa Rehoboamu alipofika Yerusalemu, akakusanya nyumba yote ya Yuda na kabila la Benyamini, wanaume wapiganaji 180,000, kufanya vita dhidi ya nyumba ya Israeli na kuurudisha tena ufalme kwa Rehoboamu mwana wa Solomoni. 2 Lakini neno hili laBwanalikamjia Shemaya mtu wa Mungu: 3 “Mwambie Rehoboamu mwana wa Solomoni mfalme wa […]
Category Archives: 2 Mambo ya nyakati
2 Mambo ya nyakati 12
Shishaki Ashambulia Yerusalemu 1 Baada ya nafasi ya Rehoboamu kuimarika na kuwa na nguvu, yeye na Israeli yote waliiacha sheria yaBwanaMungu. 2 Kwa sababu hawakuwa waaminifu kwaBwana, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu katika mwaka wa tano wa kutawala kwa Mfalme Rehoboamu. 3 Akiwa na magari ya vita 1,200 na wapanda farasi 60,000 na idadi […]
2 Mambo ya nyakati 13
Abiya Mfalme Wa Yuda 1 Katika mwaka wa kumi na nane wa kutawala kwake Mfalme Yeroboamu, Abiya akawa mfalme wa Yuda, 2 naye akatawala huko Yerusalemu miaka mitatu. Mama yake aliitwa Maaka, binti Urieli wa Gibeoni. Basi kulikuwa na vita kati ya Abiya na Yeroboamu. 3 Abiya aliingia vitani na jeshi la watu 400,000 wenye […]
2 Mambo ya nyakati 14
Asa Atawala 1 Hivyo Abiya akalala na baba zake naye akazikwa katika Mji wa Daudi. Asa mwanawe akaingia mahali pake kuwa mfalme na katika siku zake, nchi ikawa na amani kwa miaka kumi. 2 Asa akatenda yaliyo mema na haki machoni paBwanaMungu wake. 3 Akaziondoa madhabahu za kigeni na mahali pa juu pa kuabudia miungu, […]
2 Mambo ya nyakati 15
Asa Afanya Matengenezo 1 Roho waBwanaakamjia Azaria mwana wa Obedi. 2 Akatoka ili kumlaki Asa na kumwambia, “Nisikilizeni, Asa na Yuda wote na Benyamini.Bwanayu pamoja nanyi mkiwa pamoja naye. Kama mkimtafuta, ataonekana kwenu, lakini kama mkimwacha yeye, naye atawaacha ninyi. 3 Kwa muda mrefu Israeli walikuwa hawana Mungu wa kweli, walikuwa hawana kuhani wa kuwafundisha […]
2 Mambo ya nyakati 16
Miaka Ya Mwisho Ya Mfalme Asa 1 Katika mwaka wa thelathini na sita wa kutawala kwa Asa, Mfalme Baasha wa Israeli akaishambulia Yuda na kuujengea ngome mji wa Rama ili kumzuia ye yote asitoke wala kuingia katika nchi ya Mfalme Asa wa Yuda. 2 Ndipo Asa akachukua fedha na dhahabu kutoka katika hazina ya Hekalu […]
2 Mambo ya nyakati 17
Yehoshafati Mfalme Wa Yuda 1 Yehoshafati mwanawe akaingia mahali pake kuwa mfalme na akajiimarisha dhidi ya Israeli. 2 Akaweka jeshi katika miji yote ya Yuda yenye ngome na kuweka askari walinzi katika Yuda na katika miji ya Efraimu ile ambayo baba yake Asa alikuwa ameiteka. 3 BwanaMungu alikuwa na Yehoshafati kwa sababu katika miaka yake […]
2 Mambo ya nyakati 18
Mikaya Atoa Unabii Dhidi Ya Ahabu 1 Basi, Yehoshafati alikuwa na mali nyingi sana na heshima. Naye akafanya urafiki na Ahabu kwa mwanawe kumwoa binti wa Ahabu. 2 Baada ya miaka kadhaa akashuka kumtembelea Ahabu huko Samaria. Ahabu akachinja ng’ombe na kondoo wengi kwa ajili yake na watu aliokuwa amefuatana nao. Kisha Ahabu akamshawishi Yehoshafati […]
2 Mambo ya nyakati 19
Mwonaji Yehu Amkemea Yehoshafati 1 Mfalme Yehoshafati wa Yuda akarudi salama kwenye jumba lake la kifalme huko Yerusalemu. 2 Yehu mwonaji, mwana wa Hanani, akapanda kwenda kuonana naye akamwambia Mfalme Yehoshafati, “Je, utawasaidia waovu na kuwapenda wale wanaomchukiaBwana? Kwa sababu ya jambo hili, ghadhabu yaBwanaiko juu yako. 3 Hata hivyo, kuna mema yaliyoonekana kwako, kwa […]
2 Mambo ya nyakati 20
1 Ikawa baada ya jambo hili, Wamoabu na Waamoni, pamoja na baadhi ya Wameuni wakaja ili wapigane vita na Yehoshafati. 2 Watu fulani wakaja wakamwambia Yehoshafati, “Jeshi kubwa linakuja dhidi yako toka Edomu na ng’ambo ya Bahari. Tayari wako Hasason-Tamari” (ndio En-Gedi). 3 Yehoshafati akaogopa, akaazimu kumtafutaBwana, akatangaza kwa Yuda wote kufunga. 4 Watu wa […]