Kutoka 21

1 “Hizi ndizo sheria utakazoweka mbele ya Waisraeli: Watumishi Wa Kiebrania 2 “Kama ukimnunua mtumwa wa Kiebrania, atakutumikia kwa miaka sita. Lakini katika mwaka wa saba, atakuwa huru naye atakwenda zake pasipo kulipa cho chote. 3 Kama akija peke yake, atakwenda huru peke yake, lakini kama akija na mke, ataondoka pamoja naye. 4 Kama bwana […]

Kutoka 22

Ulinzi Wa Mali 1 “Kama mtu akiiba maksai au kondoo na kumchinja au kumwuza, ni lazima alipe ng’ombe watano badala ya maksai mmoja na kondoo wanne badala ya kondoo mmoja. 2 “Kama mwizi akishikwa anavunja nyumba akapigwa hata akafa, aliyemwua hana hatia ya kumwaga damu; 3 lakini jambo hilo likitokea wakati jua limechomoza, huyo mtu […]

Kutoka 23

Sheria Za Haki Na Rehema 1 “Usieneze habari za uongo. Usimsaidie mtu mwovu kwa kuwa shahidi mwenye nia ya kudhuru wengine. 2 “Usifuate umati wa watu katika kutenda mabaya. Unapotoa ushahidi kwenye mashtaka, usipotoshe haki ukijumuika na umati wa watu, 3 nawe usimpendelee mtu maskini katika mashtaka yake. 4 “Kama ukikutana na maksai au punda […]

Kutoka 24

Agano Lathibitishwa 1 Kisha Mungu akamwambia Mose, “Njoni huku juu kwaBwana, wewe na Aroni, Nadabu na Abihu, pamoja na wazee sabini wa Israeli. Mniabudu kwa mbali, 2 lakini Mose peke yake ndiye atakayemkaribiaBwana; wengine wasije karibu. Nao watu wasije wakapanda pamoja naye.” 3 Mose alipokwenda na kuwaambia watu maneno yote na sheria zote zaBwana, wakaitikia […]

Kutoka 25

Sadaka Kwa Ajili Ya Maskani Ya Mungu 1 Bwanaakamwambia Mose, 2 “Waambie Waisraeli waniletee sadaka. Utapokea sadaka kwa ajili yangu kutoka kwa kila mtu ambaye moyo wake wapenda kutoa. 3 Hizi ndizo sadaka utakazozipokea kutoka kwao: dhahabu, fedha na shaba; 4 nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, pamoja na nguo […]

Kutoka 26

Maskani Ya Mungu 1 “Tengeneza Hema kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi atatarizi makerubi kwenye mapazia hayo. 2 Mapazia yote yatakuwa na ukubwa mmoja: kila moja litakuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nanena upana wa dhiraa nne. 3 […]

Kutoka 27

Madhabahu Ya Sadaka Ya Kuteketezwa 1 “Jenga madhabahu ya mbao za mti wa mshita, kimo chake ni dhiraa tatu;itakuwa mraba, urefu wake dhiraa tanona upana wake dhiraa tano. 2 Tengeneza upembe kwenye kila pembe ya hizo pembe nne, ili kwamba zile pembe na madhabahu ziwe zimeungana na uifunike madhabahu kwa shaba. 3 Tengeneza vyombo vyake […]

Kutoka 28

Mavazi Ya Kikuhani 1 “Mtwae Aroni ndugu yako aliyeletwa kwako kutoka miongoni mwa Waisraeli, pamoja na wanawe Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari, ili wanitumikie katika kazi ya ukuhani. 2 Mshonee Aroni ndugu yako mavazi matakatifu ili yampe ukuu na heshima. 3 Waambie mafundi stadi wote niliowapa hekima katika shughuli hiyo wamtengenezee Aroni mavazi hayo, ili […]

Kutoka 29

Kuweka Wakfu Makuhani 1 “Hili ndilo utakalofanya ili kuwaweka wakfu makuhani ili wanitumikie mimi katika kazi ya ukuhani: Chukua fahali mchanga mmoja na kondoo waume wawili wasio na dosari. 2 Kutokana na unga laini wa ngano usiotiwa chachu, tengeneza mikate na maandazi yaliyokandwa kwa mafuta, pamoja na mikate midogo myembamba. 3 Viwekwe vyote ndani ya […]

Kutoka 30

Madhabahu Ya Kufukizia Uvumba 1 “Tengeneza madhabahu ya mti wa mshita kwa ajili ya kufukizia uvumba. 2 Madhabahu iwe mraba, urefu na upana wa dhiraa mojana kimo cha dhiraa mbili, pembe zake zitakuwa za kitu kimoja nayo. 3 Funika juu ya hiyo madhabahu, na pande zote na pembe zake kwa dhahabu safi, na ufanyize ukingo […]